sw_tn/act/20/28.md

1.0 KiB

Kwa sababu hiyo

Neno hili ni alama ya kauli inayosema kwa sababu ya kile ambacho nilisema hapo awali. Katika kesi hiyo, inaturudisha nyuma kwa yale yote ambayo Paulo amesema hadi sasa katika hotuba yake kuhusu yeye kuondoka kwao.

juu ya kundi lolote ambalo Roho Mtakatifu amewaweka ninyi kuwa waangalizi. Iweni waangalifu kulichunga kusanyiko la Bwana

Waumini wanafananishwa na kundi la kondoo. Viongozi wamepewa wajibu na Mungu kulilinda kundi la waumini kwa uangalifu mkuu dhidi ya mbwa mwitu.

kusanyiko la Bwana, ambalo alilinunua kwa damu yake mwenyewe

kumwaga "damu" ya Kristo hapa inafananishwa na malipo kwa Mungu kwa ajili ya dhambi zetu.

mbwa mwitu wakali wataingia kwenu, na wasilihurumie kundi.

Ni picha ya waumini ambao ni kondoo kuanza kufundishwa mafundisho ya uongo yatakayoanza kuwavutana kuwatoa katika kweli ya Mungu

ili kuwavuta wanafunzi wawafuate wao

Mwalimu wa uongo anayeweza kuwavuta waumini kwa mafundisho ya uongo, kwa lengo la kuwaondoa waumini kuwa wanafunzi wa Yesu na kuwafanya kuwa wanafunzi wake.