sw_tn/act/13/09.md

1.1 KiB

Sentensi unganishi

Wakati wakiwa katika kisiwa cha Pafo, Pauli alianza kuzungumza na Elima.

Lakini Sauli aliyeitwa Paulo

"Sauli" ambalo ni jina la Kiyahudi, na "Paulo" ambalo ni jina la Kirumi. Wakati alipokuwa akizungumza na mtawala wa Rumi, alikuwa akitumia jina la Kirumi.

akamkazia macho

"Akamkazia macho kwa makini"

Ewe mwana wa Ibilisi

Paulo anasema yule mtu alikuwa akitenda kama Ibilisi. "Wewe sawa na shetani" au "Unatenda kama Shetani"

umejazwa na aina zote za udanganyifu na uovu

"Wakati wote unatenda kwa kusababisha wengine waamini ambacho si kweli kwa kutumia udanganyifu na mara zote unatenda mabaya"

Uovu

Inamaanisha kuwa mzembe na kutokufuata sheria ya Mungu kwa dhati.

Wewe ni adui wa kila aina ya haki

Paulo anamwunganisha Elima pamoja na Ibilisi. Kama vile Ibilisi ni adui wa Mungu kwa kuwa kinyume na haki, ndivyo ilivyo kwa Elima pia.

Hautakoma kuzigeuza njia za Bwana, zilizonyooka, je utaweza?

Paulo anatumia swali kumkemea Elima kwa upinzani wake kwa Mungu.

njia za Bwana, zilizonyooka

Hapa "njia zilizonyoka" linamaanisha njia zilizo za kweli katika Bwana.