sw_tn/act/01/24.md

862 B

Waliomba wakisema

"Ndipo waumini waliomba" Inamaanisha wote waliokuwemo chumba cha juu waliomba, pengine kwa kuongozwa na mtume mmoja.

Wewe, Bwana, wajua mioyo ya watu wote

"Bwana, Wewe wajua msukumo wa ndani na mawazo ya kila mmoja"

hivyo funua yupi kati ya hawa wawili ndiye uliye mteua kuchukua nafasi katika huduma hii ya kitume

"Kwa sababu hiyo, Mungu, tuoneshe sisi yupi kwenye watu hawa wawili umemteua kujaza nafasi hii wazi katika matume"

Kutokana na Yuda kukosea na kwenda njia yake mwenyewe

Nafasi iliachwa wazi sababu Yuda alimsaliti Yesu, aliondoka, na akafa.

Wakawapigia kura

Walitumia kura kuamua kati ya Yusufu na Mathiasi

Kura ikamwangukia Mathiasi

Kura iliashiria kwamba Mathiasi alikuwa amechaguliwa kuchukua nafasi ya Yuda

Alihesabiwa pamoja na mtume kumi na mmoja

"wanafunzi walimchukulia kuwa ni mmoja wa mitume"