sw_tn/act/01/17.md

831 B

Sentensi unganishi

Katika mstari 17 Petro anaendelea na hotuba yake kwa waumini.

Maelezo ya Jumla:

Ingawa Petro anaongea na kundi lote la waumini waliokuwa chumba cha juu, lakini neno "sisi" analitumia kwa kuwataja mitume pekee waliotembea, kuketi, kuongea na Yesu tangu mwanzo wa huduma yake hadi kupaa kwake mbinguni.

Sasa mtu huyu

Neno "mtu huyu" linaelezea juu ya Yuda Iskariote.

alichokipokea kwa uovu wake

"pesa alizopokea ni malipo ya ya uovu alioufanya"

hapo alianguka akitanguliza kichwa, mwili ukapasuka na matumbo yake yote yakawa wazi yakamwagika.

Kuanguka kwa Yuda kulisababisha mwili wake kupasuka na matumbo kumwagika.

shamba la damu.

Watu waliokuwa wakiishi Yerusalemu waliposikia habari za Yuda na kifo chake, wakaliita jina lile shamba lililonunuliwa kwa fedha hizo kuwa ni shamba la damu.