sw_tn/2sa/19/34.md

1.2 KiB

Kwani kuna siku ngapi zilizosalia maishani mwangu, hata niende na mfalme huko Yerusalemu?

Hapa Berzillai anamaanisha kwamba yeye ni mzee na kwamba hakuna haja ya yeye kumsindikiza Daudi. Yaweza kumaanisha kuwa sitaweza kuishi muda mrefu. Kwa hiyo hakuna haja ya kwenda na mfalme huko Yerusalem.

Miaka themanini

"umri wa miaka 80"

Kwa nini basi mtumishi wako awe mzigo kwa bwana wangu mfalme?

Hapa Berzilai anamaanisha kwamba hapendi kuwa mzigo kwa mfalme.

Je naweza kutofautisha kati ya mema na mabaya?

Berzilai anatumia maswali kusisitiza kwa nini hapendi kwenda Yerusalemu. "Mema" na "mabaya" yanamaanisha kinachotamaniwa na kisichotamaniwa.

Je mtumishi wako aweza kuonja anachokula na kunywa?

Barizilai anatumia maswali ya kusisitiza kwa nini haitaji kwenda Yerusalemu.

Je naweza kuisia zaidi sauti za wanaume na wanawake waimbao?

Berizilai anatumia maswali ya msisitizo kwa nini hapendi kwenda Yerusalemu.

Kwa nini basi mtumishi wako awe mzigo kwa bwana wangu mfalme?

Berizilai anatumia swali kusisitiza kwamba hafikirii kwama anapaswa kwenda na mfalme huko Yerusalemu.

Kwa nini mfalme anilipe kwa thawabu hiyo?

Berizilai anatumia swali kusisitiza kwamba hajui ni lini mfalme angemlipa kwa njia hii.