sw_tn/2sa/01/21.md

1.0 KiB

Milima ya Gilboa

Daudi anaongea moja kwa moja kwa "Milima ya Gilboa" kama kwamba ilikuwa ikisikiliza wimbo wake

Haya na kusiwe na umande juu yenu

Daudi analaani ardhi alipofia Mfalme Sauli vitani. Hii ilikuwa siyo heshima kwa Sauli, aliyekuwa mfalme mtiwa mafuta wa Mungu.

ngao ya mwenye uwezo imechafuliwa

"Mwenye uwezo" hapa inaonesha kwa Sauli. Ngao ilichafuliwa kwa sababu ilianguka juu ya ardhi, na kwa sababu damu ya mfalme ilimwagwa juu yake.

Ngao ya Sauli haijatiwa mafuta tena

Ngao ya Sauli ilikuwa imetengenezwa kwa ngozi. Ili kuitunza, ilipakwa mafuta. Inaweza pia kutafsiriwa kuwa "hakuna mtu atayeijali ngao ya Sauli tena"

Kutoka katika damu yao waliouawa, kutoka miili ya wenye nguvu, upinde wa Yonathani haukurudi nyuma, na upanga wa Sauli haukurudi patupu

Sauli na Yonathani wanaoneshwa hapa kuwa wapiganaji hatari na mashujaa.

upanga wa Sauli haukurudi patupu

Upanga wa Sauli unazungumziwa kama kitu hai kwamba ungeweza kurudi wenyewe. Badala ya kurudi patupu, ulikuwa ukiwa na damu ya adui wa Sauli uliowauwa.