sw_tn/1ti/04/06.md

1.2 KiB

kama utayaweka mambo haya mbele ya ndugu

"uweke fikra hizi ndani ya akili za waumini" au "uwasaidie waumini kuyakumbuka maneno haya." "Fikra" au "maneno" yanamaanisha mafundisho.

unaendelea kulishwa

"kufundishwa". Mungu alikuwa akimfanya Timotheo mwenye nguvu na kumfundisha kuyafanya yampendezayo Mungu.

maneno ya imani

"maneno ambayo yanawasababisha au yanayowafanya watu kuamini"

hadithi za kidunia zinazopendwa na wanawake wazee

"hadithi za kidunia na za wanawake wazee." Maneno "zilizopendwa na wanawake wazee" inaweza kuwa mfano kwa maana ya "za kijinga" au "kipuuzi." Paulo hakusudii kuwatukana wanawake katika kuwaongelea kwake :wanawake wazee." Badala yake, yeye na wasikilizaji wake walijua kwamba wanaume wanakufa wakiwa vijana ukulinganisha na wanawake, kwa hiyo kuna wanawake wengi zaidi kuliko wanaume ambao akili zao zimekuwa dhaifu kwa sababu ya umri mkubwa.

jifunze kutenda kwa namna ambayo inampendeza Mungu

"jifunze kuwa wa kiMungu zaidi" au "jifunze kutenda kwa namna ua njia ambayo inampendeza Mungu" au "jitahidi kuwa wa kiMungu zaidi"

mazoezi ya mwili

"mazoezi ya kimwili"

kutakusaidia maisha ya sasa hapa duniani

"ni ya manufaa kwa maisha haya" au "inasaidia kuyafanya maisha haya kuwa bora"