sw_tn/1jn/04/17.md

1.3 KiB

Kwa sababu hii, pendo hili limekwisha kamilishwa miongoni mwetu, ili tuwe na ujasiri

Hili laweza kutamkwa katika mtindo tendaji. (Maana zinazowezekana ni 1) " Kwa sababu kwa sababu hii" hurejea 4:14 : "Kwababu yeyote akaaye katika pendo hukaa ndani ya Mungu na Mungu ndani yake, Mungu amelifanya pendo lake kamili kwa ajili yetu, na kwa hiyo tunaweza kuwa na ujasiri kamili" au 2) "Kwa sababu hii" hurejea kwa "tuwe na ujasiri." : "Tuna ujasiri kwamba Mungu atatupokea katika siku anayohukumu kila mmoja, kwa hiyo tunajua amelifanya pendo lake kuwa kamili"

pendo hili limefanywa timilifu miongoni mwetu

"hivi ndivyo ambavyo Mungu amelifanya pendo lake kuwa kamili kwa ajili yetu"

kwa sababu kama yeye alivyo, na sisi ndivyo tulivyo katika ulimwenngu huu

"kwa sababu uhusiano alionao Yesu pamoja na Mungu ni uhusiano ule ule tulionao sisi pamoja na Mungu ulimwenguni humu"

pendo kamili huitupa hofu nje

Hapa "pendo" limeelezwa kama nafsi yenye uwezo wa kuondoa hofu. Pendo la Mungu ni kamilifu, haitupasi kuogopa"

kwa sababu hofu huhusiana na hukumu

"kwa sababu tunaogopa kama tunafikiri kwamba Mungu atakapokuja atatuadhibu kila mmoja"

Lakini yeye aogopaye hajakamilishwa katika pendo.

"Mtu anapoogopa kwamba Mungu atamwdhibu yeye, inamaanisha kwamba pendo lake si kamili"