sw_tn/1jn/02/27.md

1.3 KiB

Sentensi Unganishi

Kuazia mstari 29, Yohana anatambulisha wazo la kuzaliwa kwenye familia ya Mungu. Mistari inayotangulia inaonyesha kwamba waaminio huendelea kutenda dhambi, sehamu hii inaonyesha waamini pia wana asili mpya ambayo haitendi dhambi. Inaendelea kuelezea kwamba wanaweza kutambuana kila moja.

Na kwa ajili yenu

Kifungu hiki kinamwonyesha Yohana akiwaambia pia ilivyowapasa kuishi kama wafuasi wa Yesu badala ya kuwafuata wale waliokinyume na Kristo.

yale mafuta

Humaanisha "Roho wa Mungu." Tazama maelezo katika 2:20 uone linavyofafanuliwa

mambo yote

Kirai hiki ni baalagha ambayo hutia chumvi mambo au matukio. : "kila kitu mnachohitaji kukijua"

kaeni ndani yake.

"ishini kwa ajili ajili yake." Tazama uone jinsi kurai hiki kilivyotafsiriwa katika 2:4. Jinsi mtu anavyokaa humaanisha ushirika au uhusiano wake.

Na sasa

Kirai hiki kimetumika kuunda sehemu mpya ya barua.

watoto wapendwa

Yohana alikuwa mtu mzeena kiongozi wao. Alitumia maelezo haya kuonyesha pendo lake kwao. : "watoto wangu wapendwa katika Kristo" au "ninyi mlio kama wapendwa kwangu kama wato wangu mwenyewe. Tazama ufafanuzi wake katika 2:1

atakapotokea,

"tutamwona yeye"

ujasiri

"kujiamini"

wakati atakapotokea

"atakapokuja tena"

amezaliwa na yeye.

amekuwa mzaliwa wa Mungu" au ni mtoto wa Mungu"