sw_tn/1jn/02/12.md

1.6 KiB

Maelezo ya Jumla

Yohana anaelezea sababu inayomfanya kuandika barua yake ama kwa vikundi vyenye umri mbalimbali au kwa waamini wanaotofautiana katika ukomavu. Barua yenyewe imeandikwa kwa mtindo wa kishairi.

watoto wapendwa

Yohana ni mzee na kiongozi wao. Alitumia maelezo haya kuonyesha upendo kwa aji yao. : "Watoto wangu wapendwa katika Kristo" au "ninyi mlio wapendwa kama watoto wangu mwenyewe." Tazama maelezo katika sura ya 2:1 uone linavyofafanuliwa.

dhambi zenu zimesamehewa

"Mungu husamehe dhambi zenu"

kwa ajili ya jina lake.

"jina lake" humaanisha Kristo na alivyo yeye. :"kwa sababu ya kile Kristo amefanya kwa ajili yenu"

Nawaandikia ninyi, akina baba,

Neno "akina baba" hapa linaweza kuwa fumbo au mfano ukimaanisha waamini waliokomaa. : "Ninawaandikia ninyi, waamini mlikoamaa

mnamjua

"mna uhusiano na"

yeye aliye wa tangu mwanzo.

"yeye ambaye amekuwa akiishi siku zote" au "yeye ambaye amekuwako siku zote." humaanisha Yesu au Mungu Baba."

vijana,

Hili inawezekana kumaanisha wale wasio waamini wapya tena, bali ni wale wanokua katika ukomavu wa kiroho

mko imara,

Hapa neno "imara" halimaanishi nguvu za kimwili za waamini, bali ni ule uaminifu wao kwa Kristo.

neno la Mungu linakaa ndani yenu

Mwandishi anamaanisha lile ongozeko la uaminifu wa waaminio kwa Kristo na ufahamu wao juu Yake kana kwamba alikuwa akiongelea neno la Mungu likiishi ndani yao. : "Ninyi mnaolijua neno la Mungu"

mmemshinda

Mwandishi anazungumzia juu ya maaminio kukataa kumfuata Shetani na kuipinga kwao mipango yake kana kwamba mambo hayo yamekuwa ni jambo la kumshinda yeye.