Mandhari yanahamia katika muda wa jioni ambapo Simulizi inakuwa ya Yesu kuponya watu zaidi na kufukuza mapepo..
# Maelezo ya jumla
Katika mstari wa 17, mwadishi anamnukuu nabii Isaya il ikuonesha kuwa huduma ya Yesu ilikuwa kutimiza unabii.
# Na ilipofika jioni
Hii inajulisha kwamba hii ni baada ya Sabato, kwa sababu wayahudi walikuwa hawafanyi kazi au kusafiri siku ya Sabato. Walisubiri muda wa jioni kuleta watu kwa Yesu. Hauhitaji kutaja Sabato isipokuwa unataka kuepuka tafsiri ya uongo
Hapa "neno" inamaanisha amri. Yeye aliwaamuru pepo kuondoka."
# yalitimizwa unabii wa Isaya uliyosema
Hii inaweza kuelezwa kwa mfumo hai. "Yesu alitimiza unabii kwamba nabii Isaya aliongea na watu wa Israeli."
# alichukua magonjwa yetu na kubeba malazi yetu
Mathayo anamnukuru nabii Isaya. Hii misemo miwili kiualisi inamaana moja na kusisitiza kwamba yeye aliponya magonjwa yetu yote. "aliponya wale walio wagonjwa na kuwafanya wazima."