sw_tn/gen/33/09.md

36 lines
1.3 KiB
Markdown
Raw Permalink Normal View History

2019-05-21 20:17:16 +00:00
# Ninayo ya kutosha
Neno "wanyama" au "mali" linaeleweka. "Nina wanyama wa kutosha" au "Nina mali ya kutosha"
# ikiwa nimeona kibali machoni pako
Hapa "machoni" ina maana ya fikra au mawazo ya mtu. "Kama unapendezwa na mimi"
# zawadi yangu kutoka mkononi mwangu
Hapa "mkononi" ina maana ya Yakobo. "zawadi hii nayokupatia"
# mkononi mwangu, kwa maana
Hii inaweza kutafsiriwa kama sentensi mpya. "mkono wangu. Kwa uhakika"
# nimeona uso wako, na ni kama kuona uso wa Mungu
Maana ya tashbihi hii haipo wazi. Maana zaweza kuwa 1) Yakobo amefurahi ya kwamba Esau amemsamehe kama Mungu alivyomsamehe au 2) Yakobo anashangazwa kumuona kaka yake tena kama alivyoshangazwa kumuona Mungu au 3) Yakobo ananyenyekea kuwa mbele ya Esau kama alivyonyenyekea kuwa mbele za Mungu.
# nimeona uso wako
Hapa "uso" ina maana ya Esau. Ni vyema kutafsiri kama "uso" kwa sababu ya umuhimu wa neno "uso" hapa pamoja na "uso wa Mungu" na "uso kwa uso" katika 32:29.
# uliyoletewa
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "ambazo watumishi wangu wamekuletea"
# Mungu amenitendea kwa neema
"Mungu amenitendea wema sana" au "Mungu amenibariki sana"
# Hivyo Yakobo akamsihi, na Esau akamkubali
Ilikuwa utamaduni kukataa zawadi kwanza, lakini kukubali zawadi ile baadae kabla ya mtoaji kukwazika.