sw_tn/act/16/intro.md

18 lines
926 B
Markdown
Raw Permalink Normal View History

2021-09-10 19:12:24 +00:00
# Matendo 16 Maelezo kwa jumla
2021-09-10 19:21:44 +00:00
## Dhana maalum katika sura hii
2021-09-10 19:12:24 +00:00
2021-09-10 19:21:44 +00:00
### Kutahiriwa kwa Timotheo
2021-09-10 19:12:24 +00:00
Paulo alimtahiri Timotheo kwa vile walikuwa wanahubiri ujumbe wa Yesu kwa Wayahudi na watu wa Mataifa. Paulo alitaka Wayahudi wajue kwamba aliheshimu sheria za Musa ingawa viongozi wa kanisa Yerusalemu walikuwa wameamua kwamba Wakristo hawana haja ya tohara.
2021-09-10 19:21:44 +00:00
### Mwanamke aliyekuwa na pepo wa uaguzi
2021-09-10 19:12:24 +00:00
Watu wengi hupenda sana kujua yanayojiri siku za usoni, lakini sheria za Musa zilisema kwamba ni dhambi kuongea na roho za wafu ili kujua yajayo. Inaonekana huyu mwanamke alijua kutabiri yajayo vyema.Alikuwa mtumwa aliyetumiwa na wenyeji wake kujitajirisha kutokana na kazi hii yake. Paulo alitaka aache kutenda dhambi, na kwa hivyo aliamuru huyo pepo amtoke. Luka hatuelezi iwapo alianza kumfuata Yesu ama hata jambo lingine kumhusu.
## Links:
* __[Acts 16:01 Notes](./01.md)__
2021-09-10 19:21:44 +00:00
__[<<](../15/intro.md) | [>>](../17/intro.md)__