swc_act_text_reg/27/09.txt

1 line
450 B
Plaintext

\v 9 Kisha kupitisha siku nyingi, tukafikia katika nyakati za hatari za safari ya bahari, kwa maana siku ya kufunga kula ilikuwa imekwisha kupita. Halafu Paulo akatupatia shauri hili: \v 10 «Wanaume, ninaona kwamba safari yetu itakuwa ya hatari na hasara nyingi, si kwa chombo na mizigo tu, lakini kwa maisha yetu vilevile.» \v 11 Lakini yule mkubwa wa waaskari akasadiki zaidi maneno ya kapiteni na ya mwenye chombo kuliko kufuata shauri la Paulo.