\v 22 Watu wa kanisa la Yerusalema waliposikia habari hii, wakamutuma Barnaba kwenda kule Antiokia. \v 23 Naye alipofika, akaona mambo yote yaliyotendeka kutokana na neema ya Mungu, akafurahi, naye akawatia wanafunzi wote moyo kusudi waendelee kushikamana na Bwana kwa moyo wao wote. \v 24 Barnaba alikuwa mtu mwema, mwenye kujazwa na Roho Mtakatifu na mwenye imani sana. Na watu wengi wakaongezeka kwa Bwana.