sw_num_text_reg/04/12.txt

1 line
511 B
Plaintext

\v 12 Watavichukua vyombo vyote vya kazi takatifu na kuvizonga kwenye hiyo nguo ya rangi ya samawi. Watavifunika na ngozi za pomboo na kuviweka hivyo vyombo kwenye miti ya kubebea. \v 13 Watayaondoa majivu kwenye madhabahu na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake. \v 14 Wataviweka kwenye miti ya kubebea vyombo vyote wanavyovitumia kwa kazi ya madhabahuni. Vyombo hivi ni vyetezo, majembe, mabakuli na vitu vingine vya madhabahuni. Wataifunika madhabahu na ngozi za pomboo na kuweka ile miti ya kubebea.