Sun Jun 26 2022 22:14:40 GMT+0300 (East Africa Time)
This commit is contained in:
commit
3ad29657f1
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 Mungu alimwambia Musa katika hema ya kukutania walipokuwa katika jangwa la Sinai. Hii ilitokea katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili miaka miwili baadaya Waisraeli kutoka nchi ya Misri. Mungu alisema, \v 2 'fanya sensa ya wanaume wote wa Israel kutoka kila ukoo, katika familia za baba zao. Wahesabu kwa majina, wahesabu kila mume, kila mwanamume \v 3 kuanzia umri a miaka ishirini na zaidi. Uwahesabu wote wanaoweza kupigana kama askari wa Israel. Wewe na Haruni mtaandika idadi ya wanaume katika makundi ya majeshi yao.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 4 Kila mwanamume kwa kila kabila, kichwa cha ukoo, lazima atumike na wewe kama kiongozi wa kabila. \v 5 Haya ndiyo majina ya viongozi ambao watapigana pamoja na wewe: Kutoka kabila la Reubeni, Elizuri mwana wa Shedeuri; \v 6 kutoka kabila la Simeoni, Shelumiel mwana wa Zurishadai
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 7 Kutoka kabila la Yuda, Nashoni mwana wa Aminadabu; \v 8 Ktoka kabila la Isakari, Nethaneli mwana wa Zuari; \v 9 kutoka kabila Zebuluni, Eliabu mwana wa Heloni
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 10 kutoka kabila la Efraimu mwana wa Yusufu, Elishama mwana wa Ammihudi; kutoka kabila la Manase, Gamaliel mwan wa Pedazuri; \v 11 kutoka kabila la Benjamini mwana wa Ysufu, Abidani mwan wa Gidion;
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 12 Kutoka kabila la Dan, Ahizeri mwana wa Amishadai; \v 13 kutoka kabila Asheri, Pagieli mwana wa Okirani; \v 14 kutoka kabila la Gadi, Eliasafu mwana wa Deuli; \v 15 na kutoka kabila la Naftali, Ahira mwana wa Enani."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 16 Hawa ndio wanaume waliochaguliwa kutoka kwa watu. Waliongoza kabila za mababu zao. Walikuwa viongozi wa koo katika Israel.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 17 Musa na Haruni wakawachukua wale wanaume, waliokuwa wameandikwa kwa majina, \v 18 na pamoja na wanaume hao waliwakusanya wanume wote katika siku ya kwanza ya mwezi wa pili. Kisha kila mwanume wa miaka ishirini na zaidi alitambua babu zake. Alitakiwa kutaja koo na famila kutoka katika ukoo. \v 19 Kisha Musa akaandika hesabu yao huko katika nyika ya Sinai, Kama Mungu alivyokuwa amemwamuru kufanya.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 20 Kutoka uzao wa Reubeni, mtoto wa kwanza wa Israel, yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka hesabu ya ukoo na familia. \v 21 Waliwahesabu wanaume 46, 000 kutoka ukoo wa Reubeni.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 22 Kutoka uzao wa Simeoni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini na zaidi au wenye uwezo wa kwenda vitani, kutokana na hesabu ya ukoo na familia. \v 23 Walihesabu wanaume 59, 300 kutoka kabila la Simeoni.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 24 Kutoka uzao wa Gadi yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia. \v 25 Walihesabu wanaume 45, 650 kutoka kabila la Gadi.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 26 Kutoka uzao wa Yuda yalihesabiwa majina yote ya wanaume wenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia. \v 27 walihesabiwa wanume 74, 000 kutoka kabila la Yuda.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 28 Kutoka uzao wa Isakari yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia. \v 29 Walihesabiwa wanaume 54, 000 kutoka kabila la Isakari.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 30 Kutoka uzao wa Zabuloni yalihesabiwa majina yote ya kila mwanamume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia. \v 31 Walihesabiwa wanume 57, 400 kutoka kabila la Zabuloni.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 32 Kutoka uzao wa Efraimu mwana wa Yusufu yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia. \v 33 Walihesabiwa wanaume 40, 500 kutoka kabila la Efraimu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 34 Kutoka uzao wa Manase mwana wa Yusufu yaliheabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia. \v 35 Walihesabiwa wanaume 32, 000 kutoka kabila la Manase.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 36 Kutoka uzao wa Benjamini yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na wenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia. \v 37 Walihesabiwa wanaume 35, 000 kutoka kabila la Benjamini.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 38 Kutoka uzao wa Dani yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, Kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia. \v 39 Walihesabiwa wanaume 62, 000 kutoka kabila la Dani.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 40 Kutoka uzao wa Asheri yalihesabiwa majina yote ya kila mwanume mwenye umri wa miaka ishirini au zadi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu y a ukoo na familia. \v 41 Walihesabiwa wanaume 41, 500 kutoka ukoo wa Asheri.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 42 Kutoka ukoo wa Naftali yalihesabiwa majina yote ya kila mwanaume mwenye umri wa miaka ishirini au zaidi na mwenye uwezo wa kwenda vitani, kutoka kwenye hesabu ya ukoo na familia. \v 43 Walihesabiwa wanaume 53, 400 kutoka kabila la Naftari
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 44 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote hawa, pamoja na wale wanaume kumi na wawili waliokuwa wakiongoza yale makabila kumi na mawili ya Israeli. \v 45 Kwa hiyo wanaume wote wa Israeli wenye umri wa miak ishirini au zaidi, wote wenye uwezo wa kwenda vitani, walihesabiwa kutoka kwenye familia zao. \v 46 Walihesabu wanaume 603, 550.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 47 Lakini wanaume toka uzao wa Lawi hawakuhesabiwa, \v 48 Kwa sababu BWANA alimwambia Musa, \v 49 "usiwahesabu wale wa kabila la Lawi wala kuwajumuisha kwenye jumla ya watu wa Israeli.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 50 Badala yake, waagize Walawi kuliangalia hema la amri za agano, na kuangalia mapambo ya hema na vyote vilivyomo. Walawi watalazimika kulibeba hema na lazima wayabebe mapambo ya hema. Lazima waliangalie hema na kuyatengeneza mazingira yake. Wataiangalia masikani na kuzitengeneza kambi zinazolizunguka.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 51 Kila hema litakapotakiwa kuhamishiwa eneo jingine, Walawi ndio watakaolipeleka pale. Na kila hema litakapotakiwa kusimamishwa, Walawi ndio watakao lisimamisha. Na mgeni yeyote atakayelisogelea hema lazima auawe. \v 52 Wakati watu wa Israeli watakaposimamisha hema zao, kila mwanaume lazima awe karibu na bango la jeshi lake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 53 Hata hivyo Walawi lazima waweke hema zao kuizunguka hiyo masikani ya amri za agano ili kwamba hasira yangu isije ikawaka juu ya wana wa Israeli. Walawi lazima wailinde hiyo masikani ya amri za agano." \v 54 Wana wa Israeli walifanya yote haya. Walifanya yote ambayo BWANA aliagiza kupitia Musa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 BWANA akasema na Musa na Haruni tena. Akamwambia, \v 2 Kila mtu atapanga kulingana na mahali pake, pamoja na mabango ya baba zao. Watapanga kuzunguka hema ya kukutania kila upande.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 3 Wale watakaopanga mashariki mwa hema ya kukutania, mahali ambapo juu huonekana wakati wa jua kuchomoza, ni makambi ya Yuda nao watakuwa katika kundi lao. Nashoni mwana wa Aminadabu ni kiongozi wa watu wa Yuda. \v 4 Idadi ya watu wa Yuda ni 74, 600.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 5 Kabila la Isakari litapanga mbele ya Yuda. Nethaneli mwana wa Zuari ataliongoza jeshi la Isakari. \v 6 Idadi ya kikosi chake ni wanaume 54, 000.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 7 Kabila la Zabuloni litapanga mbele ya Isakari. Eliabu mwana wa Heloni ndiye atakayeliongoza jeshi la Zabuloni. \v 8 Idadi ya kikosi chake ni 57, 400.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 9 Idadi yote ya kambi y a Yuda ni 186, 400. Watakuwa wa kwanza kuondoka.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 10 Upande wa kusini kutakuwa na kambi ya Reubeni katika kundi lao. Kiongozi wa kundi la Reubeni ni Elizuri mwana wa Shedeuri. \v 11 Idadi ya kikosi chake ni 46, 500.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 12 Simeoni atapanga mbele ya Reubeni. Kiongozi wa watu wa Simeoni ni Shelumieli mwana wa Zurishadai. \v 13 Waliohesabiwa kwenye kikosi chake ni 59, 300.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 14 Kabila la Gadi litafuatia. Kiongozi wa watu wa Gadi ni Eliasafu mwana wa Deuli. \v 15 Idadi ya kikosi chake ni 45, 650.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 16 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Reubeni, kulingana na kikosi chake, ni 151, 450. Watakuwa wa pili kuondoka.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 17 Kifuatacho, ni hema la kukutania kuondoka kambini pamoja na Walawi likiwa katikati ya kambi zote. Lazima waondoke hapo kambini kwa mpangilio huo kama walivyoingia kwenye kambi. Kila mwanamume lazima awe mahali pake kwa kufuata bango lake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 18 Migawanyiko ya kambi y Efraimu kufuata mahali pake. Kiongozi wa watu wa Efraimu ni Elishama mwana wa Amihudi. \v 19 Hesabu ya kikosi hiki ni 40, 500.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 20 Baada ya hao lilifuata kabila la Manase. Kiongozi wa Manase ni Gamaliel mwana wa Pedazuri. \v 21 Hesabu ya kikosi hiki ni 32, 200.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 22 Kabila litakalofuata ni la Benjamini. Kiongozi wa Benjamini n Abidani mwana wa Gidioni. \v 23 Hesabu ya kikosi hiki ni 35, 000
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 24 Wote waliohesabiwa katika kambi ya Efraimu ni 108, 100. Watakuwa wa tatu kuondoka.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 25 Upande wa kaskazini kutakuwa na kambi ya kikosi cha Dani. Kiongozi wa watu wa Dani ni Ahiezeri mwana wa Amishadai. \v 26 Hesabu ya kikosi hiki ni 62, 700.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 27 Watu wa kabila ya Asheri watapanga mbele ya Dani. Kiongozi wa Asheri ni Pagieli mwana wa Okirani. \v 28 Hesabu ya Kikosi hiki ni 41, 500.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 29 Kabila la Naftali ndilo litakalofuatia. Kiongozi wa Naftali ni Ahira mwana wa Enani. \v 30 Hesabu ya kikosi hiki ni 53, 400.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 31 Wote waliohesabiwa kwenye kambi ya Dani ni 157, 600. Hawa watakuwa wa mwisho kuondoka kambini, wakifuata bango lao.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 32 Hawa ndio Waisraeli, waliohesabiwa kufuata familia zao. Wote waliohesabiwa kwenye kambi zao, kwa kufuata vikosi vyao ni 603, 550. \v 33 Lakini Musa na Haruni hawakujumuisha Walawi kwenye Hesabu ya Waisrael. Ilikuwa kama BWANA alivyokuwa amemwagiza Musa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 34 Watu wa Israel walifanya yote ambayo BWANA alimwagiza Musa. Walipanga kwa kufuata mabango yao. Walisafiri kutoka kambini kwa kufuata jamaa zao, kwa mpangilio wa familia za koo zao.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 Sasa hii ndiyo historia ya uzao wa Haruni na Musa wakati BWANA aliposema na Musa kwenye mlima Sinai. \v 2 Majina ya watoto wa Haruni walikuwa Nadabu ambaye ndiyo mtoto wa kwanza, na Abihu, na Eliezeri, na Ithamari.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 3 Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni, makuhani waliokuwa wamepakwa mafuta na kuwekwa wakfu kutumika kama makuhani. \v 4 Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya BWANA walipomtolea moto usiokubalika walipokuwa katika nyika ya Sinai. Nadabu na Abihu hawakuwa na watoto, kwa hiyo Eliazari na Ithamari walitumika kama makuhani pamoja na baba yao.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 5 BWANA alinena na Musa, akamwambia, \v 6 "Walete kabila ya Lawi na uwaweke kwa Haruni kuhani ili wamsaidie
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 7 Nao lazima wafanye majukumu badala ya Haruni na jumuiya yote mbele ya hema ya kukutania. Lazima watumike hemani. \v 8 Watayatunza mapambo ya hema ya kukutania, na watawatumikia makabila ya Israel kwa huduma ya hemani.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 9 Uwaweke Walawi kwa Haruni na watoto wake. Nimewatoa kikamilifu ili wamsaidie kuwatumikia watu wa Israel. \v 10 Umchague Haruni na watoto wake kuwa makuhani, lakini mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 11 BWANA alinena na Musa. akamwambia, \v 12 "Tazama, nimewachagua Walawi katika watu wa Israel. Nimefanya hivyo badala ya kuchukua mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wana wa Israel. Hawa Walawi ni wangu. \v 13 Na hata wazaliwa wa kwanza ni mali yangu. Katika siku ambyo niliwavamia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, Niliwatenga wazaliwa wa kwanza wa Israeli kwa ajili yangu, watu na wanyama pia. Ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 14 BWANA alinena na Musa katika nyika ya Sinai. Akasema, \v 15 "Wahesabu uzao wa Lawi katika kila familia, katika nyumba za koo zao. Hesabu kila mume kuanzia mwezi mmoja au zaidi." \v 16 Musa aliwahesabu, kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 17 Majina ya watoto waLawi yalikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari. \v 18 Ukoo uliotokana na watoto wa Gerishoni walikuwa ni Libni na Shimei. \v 19 Ukoo uliotokana na watoto Kohathi walikuwa ni Amramu na, Izihari, Hebroni, na Uzieli. \v 20 Ukoo uliotokana na watoto wa Merari walikuwa ni Mahili na Mushi. Hizi ndizo koo za Walawi, zilizoorodheshwa ukoo kwa ukoo.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 21 Koo za Walibini na Washimei zilitokana na Wagerishoni. Hizi ndizo koo za Wagerishoni. \v 22 Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa na kufikia idadi ya 7, 500. \v 23 Koo za Wagerishoni watapanga upande wa magharibi wa hema.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 24 Eliasafu mwana wa Laeli ataongoza koo za uzao wa Wagerishoni. \v 25 Familia ya Gerishoni watalilinda hema la kukutania pamoja na hiyo masikani. Watalilinda hema, kifuniko chake, na lile pazia la lango la hema ya kukutania. \v 26 Wataulinda ua, lile pazia la kwenye lango--ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu. Watazilinda kamba za hema ya kukutania na vyote vilivyomo.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 27 Koo zifuatazo zinatokana na Kohathi: ukoo wa Waamrami, ukoo wa Waizihari ukoo wa Wahebroni, na ukoo wa Wauzieli. Koo hizi zinatokana na Wakohathi. \v 28 Wanaume 8, 600 wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa ili kulinda vitu vya BWANA. \v 29 Familia ya uzao wa Kohathi watapanga upande wa kusini wa Hema.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 30 Elizafani mwana wa Uzieli ndiye atakayeongoza ukoo wa Wakohathi. \v 31 Watalilinda sanduku, meza, vikalishio vya taa, madhabahu, vitu vitakatifu ambvyo hutumika katika huduma yao, pazia, na kazi zote zinazoambatana na hema. \v 32 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza wanaume wanaowaongoza Walawi. Atawasimamia wanaume wanaongoza eneo takatifu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 33 Koo mbili zimetoka kwa Merari: Ukoo wa Mahili na ukoo wa Mushi. Koo hizi zimetokana na Merari, \v 34 Wanaume 6, 200 wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi walihesabiwa. \v 35 Zurieli mwana wa Abihaili ataongoza ukoo wa Merari. Hawa watapanga upande wa kaskazini mwa hema.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 36 Uzao wa Merari utatunza mbao za hema, mataruma, nguzo, makalishio, viifaa vya ujenzi na vitu vyote vinavyohusika, \v 37 na nguzo za ua zinazozunguka hema, makalishio, vigingi na kamba zake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 38 Musa na Haruni na watoto wake watapanga upande wa mashariki wa masikani, mbele ya hema ya kukutania kuelekea mawio ya jua. Wao wataajibika na majukumu ya mahali patakatifu na majukumu ya wana wa Israeli. Mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe. \v 39 Musa na Haruni wakawahesabu wanaume wote wa ukoo wa Walawi walikuwa na umri wa mwezi mmoja na zaidi, kama vile BWANA alivyokuwa ameagiza.. Walihesabu wanaume ishirini na mbili elfu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 40 BWANA alisema na Musa, "Wahesabu wanaume wote ambo ni wazaliwa wa kwanza wa Israeli ambao wana umri wa mwezi mmoja na zaidi. Orodhesha majina yao. \v 41 Unitwalie walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli, Mimi ndimi BWANA. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa uzao wa Israeli,"
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 42 Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli kama BWANA alivyomwagiza kufanya. \v 43 Aliwahesabu wazaliwa wote wa kwanza kwa mjina, wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi. Alihesabu wanaume 22, 273.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 44 Tena BWANA alinena na Musa. Akasema, \v 45 "Watwae Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa wana wa Israeli. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wanyama wa Waisreli wengine. Walawi ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 46 Unikusanyie shekeli tano za wokovu kwa kila hao 273 za hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli za hao wanaozidi idadi ya Walawi. \v 47 Utazitumia hizo shekeli tano kwa kipimo cha mahali patakatifu. Shekeli moja ni sawa na gera ishirini. \v 48 Utawalipa hizo shekeli za wokovu kwa Haruni na wanawe." \v 49 Kwa hiyo Musa akakusanya shakeli za wokovu kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliookolewa na Walawi. \v 50 Musa akakusanya zile fedha kutoka kwa hao wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli. Alikusanya jumla ya shekeli 1, 365, zenye kipimo sawa na mahali patakatifu. Musa akamlipa Haruni na wanawe hizo shekeli za wokovu. \v 51 Musa akafanya kila kitu alichoagizwa na neno la BWANA kama BWANA alivyomwagiza.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema, \v 2 Fanya sensa ya uzao waume wa Kohathi kutoka kwa Walawi, kwa kufuata jamaa na na familia za koo. \v 3 Uwahesabu wanaume ambao wana umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Hawa wataungana na kundi linalotumika kutoa huduma kwenye hema ya kukutania. \v 4 Uzao wa Kohathi watalinda vile vitu vitakatifu zaidi vilivyohifadhiwa kwa ajili yangu katika hema ya kukutania.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 5 Wakati kambi inapojiandaa kusonga mbele, Haruni na wanawe lazima waende hemani, kulishusha pazia linalotenganisha mahali patakatifu na kulifunika sanduku la ushuhuda kwa pazia hilo. Watalifunika hilo sanduku kwa ngozi za pomboo. \v 6 Watatandika juu yake nguo za rangi ya samawi. Watachomeka hiyo miti ya kubebea.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 7 Watatandika nguo ya rangi ya samawi kwenye meza ya mikate ya wonyesho. Juu yake wataweka sahani, vijiko, mabakuli na vikombe vya kumiminia. Mikate itakuwepo daima mezani. \v 8 Wataifunika na nguo ya rangi nyekundu na ngozi za pomboo. na kuweka miti ya kubebea.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 9 Watachukua nguo ya rangi ya samawi na kukifunika kinara, pamoja na taa zake, na koleo zake, na sahani zake na vikombe vyake vya kuwekea mafuta ya taa. \v 10 Wataweka kinara na vifaa vyake vikiwa vimefunikwa na ngozi ya pomboo, na wataweka kwenye miti ya kukibebea. \v 11 Watafunika na nguo ya samawi katika madhabau ya dhahabu. Wataifunika na ngozi za pomboo, na kuweka ile miti ya kubebea.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 12 Watavichukua vyombo vyote vya kazi takatifu na kuvizonga kwenye hiyo nguo ya rangi ya samawi. Watavifunika na ngozi za pomboo na kuviweka hivyo vyombo kwenye miti ya kubebea. \v 13 Watayaondoa majivu kwenye madhabahu na kutandika nguo ya rangi ya zambarau juu yake. \v 14 Watavieka kwenye miti ya kubebea vyombo vyote wanavyovitumia kwa kazi ya madhabahuni. Vyombo hivi ni vyetezo, majembe, mabakuli na vitu vingine vya madhabahuni. Wataifuniks madhabahu na ngozi za pomboo na kuweka ile miti ya kubebea.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 15 Wakati Haruni na wanawe walipokuwa wamekamilisha kupafunika mahali patakatifu na vyombo vyote, na kambi itakapoanza kuendelea mbele, ndipo wana wa Kohathi watakapokuja kubeba vitu vya mahali patakatifu. Kama watagusa vyombo vitakatifu, lazima watakufa. Hii ni kazi ya wana wa uzao wa Kohathi, kubeba mapambo ya hema ya kukutania. \v 16 Eliazari mwana wa Haruni kuhani atalinda na kusimamia mafuta ya taa, ubani mzuri, sadaka za mara kwa mara na mafuta ya upako. Atasimamia ulinzi wa hema lote na vyote vilivyomo, mahali patakatifu na vyombo vyake."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 17 BWANA akanena na Musa na Haruni. Akasema, \v 18 Usiruhusu kabila la Wakohathi kuondolewa kati ya Walawi. \v 19 Walinde waishi ili wasije wakafa, kwa kufanya hivi. Wanapokuwa wanasogelea \v 20 wasije wakaingia ndani ili kuona eneo takatifu hata kwa kitambo, vinginevyo watakufa. Bali Haruni na wanawe wanaweza kuingia, ndipo Haruni na Wanawe watakapowapangia Wakohathi kazi maalumu ya kufanya, kwa kila mmoj."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 21 BWANA akanena na Musa tena, Akasema, "Fanya sensa kwa wana Gerishoni pia, kwa kufuata familia za mababu zao, koo zao. \v 22 Uwahesabu wale wenye umri wa mika thelathini hadi miaka hamsini. \v 23 Uwahesabu wote ili waje kuungana na wale wanaotumika katika hema ya kukutania.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 24 Hii ndiyo itakuwa kazi ya koo za Gerishoni, wanapotumikia na wanachobeba. \v 25 Watabeba pazia la masikani, hema la kukutania, na vifunikio vyake, vifuniko vya ngozi ya pomboo ambvyo viko juu yake, na pazia kwenye lango la hema ya kukutania. \v 26 Watabeba pazia la ua, pazia la kwenye mlango wa ua, ambao uko karibu na maskani karibu na madhabahu, kamba zake na vifaa vyote vya utumishi wake. Chochote kinachotakiwa kufanywa kutokana na vitu hivi, wao ndio watakaofanya.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 27 Haruni na wanawe ndio watakaongoza utumishi wa uzao wa Wagerishoni, kwa vitu vyote vile vya kusafirisha, na katika utumishi wao wote. Lazima uwagawie majukumu yao yote. \v 28 Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa wana wa Wagerishoni katka hema ya kukutania. Ithamari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza katika utumishi.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 29 Utawahesabu uzao wa Merari kwa koo zao, na uwapange katika familia za mabau zao, \v 30 kuanzia wenye umri wa miaka thelatini hadi miaka hamsini. Umuhesabu kila atakayeungana na kundi lenye utumishi katika hema ya kukutania.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 31 Huu ndio wajibu na kazi yao katika utumishi wao kwenye hema ya kukutania. Watazilinda mbao za maskani, mataluma yake, nguzo na makalishio yake, \v 32 pamoja na nguzo za ua zinazozunguka masikani, makalishio yake, vigingi na kamba zake, na vifaa vinginevya ujenzi. Waorodheshe kwa majina na majukumu yao.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 33 Huu ndio utumishi wa koo za uzao wa Merari, ambao wanatakiwa kufanya katika hema ya kukutania, chini ya uongozi wa Ithmari mwana wa Haruni kuhani."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 34 Musa na Haruni na viongozi wa watu waliwahesabu wana wa uzao wa Wakohathi kwa kufuata koo za familia za mababu zao. \v 35 Waliwahesabu wale wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. Walimhesabu kila mmoja aliyepaswa kuungana na kundi linalotoa huduma ya utumishi kwenye hema ya kukutania. \v 36 Waliwahesabu wanaume 2, 750 kwa kufuata koo zao.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 37 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume wote kutoka koo na familia za Wakohathi ambao hutumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi kwa kumtii BWANA aliyewaagiza kupitia kwa Musa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 38 Uzao wa Gerishoni walihesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao, \v 39 kuanzia umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kwa kila mmoja aliyetakiwa kuungana na watu wanaotoa huduma kwenye hema ya kukutania. \v 40 Wanaume wote waliohesabiwa kufuata koo na familia za mababu zao walikuwa 2, 630.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 41 Musa na Haruni walizihesabu koo za uzao wa Gerishoni ambao watatumika kwenye hema ya kukutania. Walifanya hivi ili kutii ambacho BWANA aliwaamuru kufanya kuptia kwa Musa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 42 Uzao wa Merari walihesabiwa kwa koo kupitia familia za mababu zao, \v 43 kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini, kila anayepaswa kuungana na watu wanaotumika kwenye hema ya kukutania. \v 44 Wanaume wote waliohesabiwa kupitia koo za familia za mababu zao walikuwa 3. 200.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 45 Musa na Haruni waliwahesabu wanaume hawa, uzao wa Merari. Kw kufanya hivi walitii amri ya BWANA aliyowaaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 46 Kwa hiyo Musa na Haruni na viongozi wa Israeli waliwahesabu Walawi wote kw kufuata koo na familia za mababu zao \v 47 kuanzia wenye umri wa miaka thelathini hadi miaka hamsini. walimhesabu kila aliyepaswa kufanya kazi kwenye masikani, na kila aliyepaswa kubeba na kulinda vitu vya kwenye hema ya kukutania. \v 48 Waliwahesabu wanaume 8, 580.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 49 Kwa agizo la BWANA, Musa alimhesabu kila mwanamume na kutunza kumbukumbu ya kazi ambayo kila mmoja anaweza kufanya. Kwa hivyo, walitii kile ambacho BWANA alikuwa amewaagiza kufanya kupitia kwa Musa.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 BWANA alinena na Musa. Akasema, \v 2 "Waamuru wana wa Israel wawatoe watu wote wenye magonjwa ya ngozi yanayoambukiza, na kila mwenye mwenye vidonda vinavyotoa harufu, na ambaye amenajisika kwa kugusa maiti. \v 3 Awe mme au mke, umtoa kambini. Ili wasije wakaitia unajisi kambi, kwa sababu Mimi huishi ndani yake," \v 4 Watu wa Israeli walifanya hivyo. Waliwatoa kambini, Kama BWANA alivyomwagiza Musa. Watu wa Israeli walimtii BWANA.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 5 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema, \v 6 "Nena na wana wa Israeli. mtu mume na mtu mke akifanya dhambi yeyote ambayo watu hufanyiana wao kwa wao, na mtu huyo akamwasi BWANA, mtu huyo atakuwa na hatia. \v 7 Ndipo huyo mtu ataungama hiyo dhambi aliyoifanya. Mtu huyo atarudisha malipo ya hatia yake na kuongeza kwenye malipo hayo sehemu ya tano zaidi. Atamlipa huyo aliyemtendea makosa
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 8 Lakini kama huyo mtu huyu aliyetendewa kosa hana ndugu wa kupokea hayo malipo, basi atalipa hayo malipo ya hatia kwangu kupitia kuhani pamoja na kondoo dume kwa ajili ya sadaka yake mwenyewe. \v 9 Kila sadaka ya wana wa Israeli, vitu ambavyo vimetengwa na vikaletwa kwa kuhani na watu wa Israeli, vitakuwa vyake. \v 10 Sadaka ya kila mtu itakuwa ya kuhani; kama mtu yeyote atatoa kitu chochote kwa kuhani, kitakuwa chake."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 11 Tena BWANA akanena na Musa. Akasema, \v 12 "Nena na wana wa Israel. Uwaambie, 'kama mke wa mtu ataasi na kufanya dhambi dhidi ya mume wake.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 13 Halafu mtu mwingine akalala naye. Kwa sababu, hiyo atakuwa amenajisika. Na hata kama mume wake hakuona na hajui, hata kama hakuna mtu aliyemkamta akiwa katika tendo na hakuna mtu wa kushuhudia dhidi yake; hata hivyo ile roho ya wivu itaendele kumjulisha yule mume kuwa mke wake amenajisika. \v 14 Ingawa, roho ya wivu inaweza kumdanganya yule mwanamume wakati mke wake hajanajisika.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 15 Kwa mazingira hayo, yule mwanamume anapaswa kumpeleka mke wake kwa kuhani. Yule mwanamume anapaswa kutoa sadaka ya divai kwa ajili yake. Atapaswa kuleta sehemu ya kumi ya efa ya unga wa shayiri. Asitie mafuta juu yake wala asitie ubani juu yake maana ni sadaka ya unga ya wivu, ni sadaka ya unga ya ukumbusho wa uovu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 16 Ndipo kuhani atasogeza karibu na kumweka mbele ya BWANA. \v 17 Kuhani atachukua kikombe cha maji matakatifu na atachukua mavumbi ya kwenye masikani. Ataweka yale mavumbi kwenye maji.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 18 Kisha kuhani atamweka huyo mwanamke mbele za BWANA na atazifungua nywele kichwani kwa huyo mwanamke. Atamwekea mikononi mwake hiyo sadaka ya unga kwa ajili ya ukumbusho, ambayo ni sadaka ya unga kwa ajili ya wivu. \v 19 Kuhani atashikilia mikononi mwake maji machungu yanayoweza kuleta laana. Kuhani atamweka huyo mwanamke chini ya kiapo na kumwambia. 'Kama haujafanya uzinzi na mwanaume mwingine, na kama hajakengeuka na kufanya uovu, basi utakuwa huru na maji haya yanayoweza kuleta laana.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 20 Lakini kama wewe, mwanamke uliye chini ya mume wako, umekengeuka, na kama umenajisika, na kama mwanamume mwingina amelala nawe, \v 21 ndipo, (kuhani atamtaka huyo mwanamke aape kiapo kinachoweza kuleta laana kwake, na kwamba ataendelea kumwambia yule mwanamke) 'BWANA atakufanya wewe kuwa laana itakayooneshwa kuwa hivyo kwa watu wako. Hii itatokea pale BWANA atakapoyafanya mapaja yako kuoza na tumbo lako kuvimba. \v 22 Haya maji ambayo huleta laana yataingia tumboni mwako na kulifanya tumbo lako kuvimba na mapaja yako kuoza,' mwanamke alitakiwa kujibu, 'Ndiyo, hayo yanipate kama mimi ni mwenye hatia.'
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 23 Naye kuhani ataziandika laana hizi kwenye kitabu, na kisha kuzifuta laana zilizoandikwa kwa maji ya uchungu.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 24 Naye kuhani atamwelekeza yule mwanamke kunywa yale maji machungu yaletayo laana. Yale maji yaletayo laana yataingia na kuwa machungu. \v 25 Kuhani ataitwaa ile sadaka ya unga ya wivu mikononi mwa yule mwanamke. Atailekeza ile sadaka ya unga mbele ya BWANA na kuileta madhabahuni. \v 26 Kuhani atachukua konzi ya sadaka ya unga mkononi mwake kama sadaka ya kuwakilisha, na kuiteketeza madhabahuni. Ndipo atakapompatia mwanamke yale maji machungu ili ayanywe.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 27 Wakati wa kumpa yale maji ili anywe, kama amenajisika kwa sababu alifanya uovu dhidi ya mume wake, ndipo yale maji yaletayo laana yatamwingia na kuwa machungu. Tumbo lake litavimba na paja lake litaoza. Yule mwanamke atalaaniwa kati ya watu wake. \v 28 Lakini kama yule mwanake hajanajisika na kama ni msafi, basi atakuwa huru. Tena ataweza kubeba uja uzito.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 29 Hii ndiyo sheria ya wivu. Ni sheria ya mwanamke anayekengeuka kwa mumewe na kunajisika. \v 30 Ni sheria ya mwanamume mwenye roho ya wivu kwa mkewe. Atamleta mwanamke mbele ya BWANA, na kuhani atamfanyia huyo mwanamke kila kitu ambacho sheria ya wivu inamtaka kufanya.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 31 Yule mwanamume atakuwa hana hatia kwa kumleta mke wake kwa kuhani. Na yule mwanmke atauchukua uovu wake."
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 1 BWANA alinena na Musa. Akamwabia, \v 2 'Nena na wana wa Israeli, uwaambie, 'Kama mume au mke ataweka nadhiri kwa BWANA kwa kiapo maalumu cha mnadhiri, ndipo atajiepusha na divai na vileo. hatakunywa siki itokanayo na divai. \v 3 Asinywe kileo kitokanacho na siki au kilevi. Asinywe maji ya divai yeyote au kula zabibu mbichi wala zilizokauka. \v 4 Katika siku zote ambazo amejitenga kwa ajili yangu, asile chochote kinachotokana na zabibu, wala kitu chochote kitokanacho na makokwa hadi maganda.
|
|
@ -0,0 +1 @@
|
|||
\v 5 Wakati wote wa nadhiri yake, wembe usiipite kichwani mwake mpaka siku zake za nadhiri kwa BWANA zitimilike. Lazima ajitenge kwa BWANA. Ataziacha nywele zake zikue kichwani mwake.
|
Some files were not shown because too many files have changed in this diff Show More
Loading…
Reference in New Issue