sw_jhn_text_reg/19/31.txt

1 line
488 B
Plaintext

\v 31 Kwa vile ilikuwa ni wakati wa maandalio, na kwa sababu miili haikutakiwa kubaki juu ya msalaba wakati wa Sabato (kwa kuwa hasa Sabato hii ilikuwa ya umuhimu), wayahudi walimwomba Pilato kuwa miguu yao wale waliokuwa wamesulibishwa ivunjwe, na kwamba miili yao ishushwe. \v 32 Ndipo askari walipokuja na kuvunja miguu ya mtu wa kwanza na wa pili aliyekuwa amesulibiwa pamoja na Yesu. \v 33 Walipomfikia Yesu, walimkuta tayari alikuwa amekwisha kufa, kwa hiyo hawakuvunja miguu yake.