sw_jer_text_reg/31/18.txt

1 line
618 B
Plaintext

\v 18 Kwa hakika nimemsikia Efraimu akilia, 'Uliniadhibu, nami nimeadhibika kama ndama asiye na mafunzo. Nirudishe nami nitarudi, kwa maana wewe ni Yahwe Mungu wangu. \v 19 Kwa maana baada ya kurudi kwako, nilikuwa na huzuni; baada ya kufundishwa, nilijipiga kofi shavu langu. Niliaibika na kudharirika, kwa maana nilizaliwa na hatia ya ujana wangu.' \v 20 Efraimu siyo mwanangu wa thamani? Yeye si mpendwa wangu, mwanangu anipendezaye? Kwa maana kila ninaponena juu yake, bado nina mwita kipenzi cha akili yangu. Kwa namna hii moyo wangu unamtamani. Kwa hakika nitakuwa na huruma juu yake—hili ni tangazo la Yahwe."