sw_jer_text_reg/44/26.txt

1 line
651 B
Plaintext

\v 26 Basi, sikiliza neno la Yahwe, Yuda yote ambao mnaishi katika nchi ya Misri, 'Ona, Nimeapa kwa jina langu kuu--asema Yahwe. Jina langu halitaitwa kwa vinywa vya wanaume wowote wa Yuda kwenye nchi ya Misri, wewe ambaye sasa unasema, "Kama Bwana Yahwe aishivyo." \v 27 Tizama, Ninawachunga kwa ajili ya maafa na si kwa wema. Kila mtu wa Yuda katika nchi ya Misri ataangamia kwa upanga na njaa mpaka watakapoisha wote. \v 28 Kisha walionusurika kwa upanga watarudi nchi ya Yuda kutoka nchi ya Misri, wakiwa idadi ndogo. Basi mabaki yote ya Yuda walioenda kwenye nchi ya Misri kuishi huko watajua ni ninani ambaye neno lake litasimama--langu au lao.