sw_jer_text_reg/33/06.txt

1 line
635 B
Plaintext

\v 6 Lakini ona, niko karibu kuleta uponyaji na tiba, kwa maana nitawaponya na nitawapa wingi wa, amani na uaminifu. \v 7 Kwa maana nitawarudisha wafungwa wao wa Yuda na Israeli; nitawajenga tena kama ilivyokuwa mwanzo. \v 8 Kisha nitawatakasa uovu wote walioufanya dhidi yangu. Nitasamehe makosa yote waliyonitenda, na njia zote walizo asi dhidi yangu. \v 9 Kwa maana mji huu kwa ajili yangu utakuwa chombo cha furaha, nyimbo, sifa na heshima kwa mataifa yote ya dunia ambao watasikia mambo yote mema ninayokwenda kufanya kwa ajili ya huu mji. Kisha wataogopa na kutetemeka kwa sababu ya mambo yote mema na amani nitakayoupa mji huu.'