sw_dan_text_reg/01/08.txt

1 line
600 B
Plaintext

\v 8 Lakini Danieli alinuia katika akili yake kuwa asingejitia ujanisi mwenyewe kwa chakula kitamu cha mfalme wala kwa divai ambayo aliinywa. \v 9 Basi, aliomba ruhusa kutoka kwa afisa mkuu ili kwamba asije akajitia uchafu yeye mwenyewe. Hivyo, Mungu alimpa Danieli kibali na huruma kupitia heshima ambayo afisa mkuu alikuwa nayo kwake. \v 10 Afisa mkuu alimwambia Danieli, "Ninamwogopa bwana wangu mfalme. Ameagiza aina ya chakula na vinywaji mnavyotakiwa kutumia. Kwa nini awaone ninyi mkiwa mnaonekana vibaya kuliko vijana wengine wa umri wenu? Mfalme aweza kukitwaa kichwa changu kwa sababu yenu.