sw_act_text_ulb/25/17.txt

1 line
530 B
Plaintext

\v 17 Kwa hiyo, walipokuja pamoja hapa, sikuweza kusubiri, lakini siku iliyofuata niliketi katika kiti cha hukumu na kuamuru mtu huyo aletwe ndani. \v 18 Wakati washitaki waliposimama kumshtaki, niliona kwamba mashataka yao hayakuonyesha uovu wowote. \v 19 Badala yake, walikuwa na mabishano fulani pamoja naye kuhusu dini yao na kuhusu Yesu ambaye alikuwa amekufa, lakini Paulo anadai kuwa yu hai. \v 20 Nilikuwa nimetatanishwa jinsi ya kuchunguza suala hili, na nikamwuliza kama angeenda Yerusalemu kuhukumiwa kuhusu mambo haya.