sw_act_text_ulb/10/30.txt

1 line
680 B
Plaintext

\v 30 Kornelio akasema, "Siku nne zilizopita, wakati kama huu, nilikuwa naomba muda wa saa tisa mchana ndani ya nyumba yangu; na tazama, mtu alisimama mbele yangu mwenye mavazi yenye kung'aa. \v 31 Akasema 'Kornelio maombi yako yamesikiwa na Mungu, na zawadi zako kwa masikini zimemkumbusha Mungu juu yako. \v 32 Hivyo tuma mtu Yafa na akamwite mtu mmoja anayeitwa Simoni aje kwako, ambaye pia huitwa Petro. Anaishi kwa mtengenezaji mmoja wa ngozi mmoja aitwaye Simoni ambaye nyumba yake iko ufukweni mwa bahari'. \v 33 Kwa hiyo mara moja nilikutuma uje. Wewe ni mwema umekuja. Sasa basi, sisi sote tupo hapa mbele za Mungu kusikia kila kitu ambacho umeangizwa na Bwana kusema."