\v 13 Alipobisha kwenye mlango wa lango, mtumishi mmoja msichana anayeitwa Roda akaja kufungua. \v 14 Alipotambua ni sauti ya Petro, kwa furaha akashindwa kuufungua mlango; badala yake, akakimbia ndani ya chumba; na kuwajulisha kuwa Petro amesimama mbele ya Mlango. \v 15 Hivyo, Wakasema kwake, "Wewe ni mwendawazimu" lakini alisisitiza kuwa ni kweli ni yeye. Wakasema "Huyo ni malaika wake."