sw_2ch_text_reg/33/04.txt

1 line
509 B
Plaintext

\v 4 Manase akajenga madhbahu za kipagani katika nyumba ya Yahwe, ingawa Yahwe alikuwa ameamuru, "Ni katika Yerusalemu ambapo jina langu litawekwa milele". \v 5 Alijenga madhabahu kwa ajili ya nyota zote za mbinguni katika vile viwanja viwili vya nyumba ya Yahwe. \v 6 Katika bonde la Beni Hinomu akawaweka wanaye katika moto. Akafanya misemo ya ubashiri, na uchawi, akasoma utabiri; akashauriana na wale waliozungumza na wafu na pepo. Akafanya maaovu mengi katika macho ya Yahwe na alimfanya Mungu akasirike.