sw_2ch_text_reg/14/01.txt

1 line
469 B
Plaintext

\c 14 \v 1 Abiya kalala pamoja na babu zake, na wakamzika katika mji wa Daudi. Asa, mwanaye, akawa mfalme katika nafasi yake. Katika siku yake nchi ilikuwa tulivu miaka kumi. \v 2 Asa alifanya yaliyomema na sahihi katika macho ya Yahwe Mungu wake, \v 3 kwa maana aliziondosha mbali madhabahu za kigeni na sehemu za juu. Akaziangusha chini nguzo za mawe na kuzikata nguzo za Maashera. \v 4 Akawaamuru Yuda kumtafuta Yahwe, Mungu wa babu zao, na kuzishika sheria na amri.