sw_dan_text_ulb/02/48.txt

1 line
384 B
Plaintext

\v 48 Ndipo mfalme alimfanya Danieli kuwa wa kuheshimiwa sana na alimpa zawadi nyingi nzuri. Alimfanya kuwa mtawala juu ya jimbo lote la Babeli. Danieli akawa liwali mkuu juu ya watu wenye hekima wa Babeli. \v 49 Danieli alipeleka ombi kwa mfalme, na mfalme aliwateua Shadraka, Meshaki na Abedinego kuwa watawala juu ya jimbo la Babeli. Lakini Danieli alisalia katika ikulu ya mfalme.