swc_mat_text_reg/23/13.txt

2 lines
588 B
Plaintext

\v 13 Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munawafungia watu wengine njia ya kuingia katika Ufalme wa mbinguni. Ninyi wenyewe hamuingii mule na zaidi ya hii munawazuiza wale wanaotaka kuingia.
[ \v 14 Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munanyanganya mali za wajane na kuomba maombi marefu kwa kujionyesha. Kwa sababu hii azabu yenu itakuwa kubwa zaidi!] \v 15 Ole kwenu, ninyi walimu wa Sheria na Wafarisayo, ninyi wanafiki! Munasafiri kuvuka bahari na inchi mbalimbali kusudi mupate kumugeuza hata mtu mmoja tu kuwa mufuasi wenu.