swc_mat_text_reg/06/05.txt

1 line
553 B
Plaintext

\v 5 Munapoomba, musikuwe kama wanafiki, kwa maana wanapenda kuomba wakisimama katika nyumba za kuabudia na pembeni ya barabara, kusudi wapate kujionyesha mbele ya watu. Kweli ninawaambia: wamekwisha kupata faida yao. \v 6 Lakini wewe, unapoomba, ingia ndani ya chumba chako, funga mulango na uombe kwa Baba yako asiyeonekana. Na Baba yako anayeona tendo unalofanya kwa siri, atakulipa. \v 7 Tena munapoomba, musitumie maneno mengi yasiokuwa na maana kama vile wapagani wanavyofanya, kwa sababu wanawaza kama Mungu atawasikia kama wakisema maneno mengi.