swc_mat_text_reg/02/13.txt

1 line
531 B
Plaintext

\v 13 Wale watu wenye elimu walipokwisha kwenda, malaika wa Bwana akamutokea Yosefu katika ndoto na kumwambia: «Amuka, utwae mtoto pamoja na mama yake na mukimbilie Misri. Mukae kule mpaka nitakapokuambia kwamba urudie, kwa maana Herode anamutafuta mtoto kusudi amwue.» \v 14 Basi Yusufu akaamuka, akamutwaa mtoto pamoja na mama yake, nao wakaondoka usiku ule kwenda Misri. \v 15 Akakaa kule mpaka Herode alipokwisha kufa, kusudi yatimie maneno haya Bwana aliyosema kwa njia ya nabii: «Nilimuita mwana wangu arudie toka Misri.»