forked from WA-Catalog/sw_tn
679 B
679 B
Luzu
Hili ni jina la mji.
El Betheli
"Jina la El Betheli lina maana ya "Mungu wa Betheli"
Mungu alikuwa amejifunua kwake
"pale Mungu alijifunua kwa Yakobo"
Debora
Hili ni jina la mwanamke.
mlezi wa Rebeka
Mlezi ni mwanamke ambaye humtunza mtoto wa mwanamke mwingine. Mlezi aliheshimika na alikuwa muhimu sana kwa familia.
Akazikwa chini kutoka Betheli
Hii inaweza kuelezwa kwa hali ya kutenda. "Walimzika chini kutoka Betheli"
chini kutoka Betheli
Msemo "chini kutoka" unatumika kwa sababu walimzika katika eneo ambalo lilikuwa chini kwa mwinuko kuliko Betheli.
Aloni Bakuthi.
"Jina la Aloni Bakuthi lina maana ya "Mwaloni ambapo kuna maombolezo"