forked from WA-Catalog/sw_tn
37 lines
1.1 KiB
Markdown
37 lines
1.1 KiB
Markdown
|
# Sentensi Unganishi
|
||
|
|
||
|
Ayubu anaendelea kuzungumza kwa rafiki zake.
|
||
|
|
||
|
# Ninyi mwasema
|
||
|
|
||
|
maneno haya yanaonesha kuwa Ayubu anawanukuu rafiki zake.
|
||
|
|
||
|
# Mungu huweka hatia ya mtu kwa ajili ya watoto wake kuilipa
|
||
|
|
||
|
Hatia inaongelewa kama kitu ambacho kinaweza kuhifadhiwa kwa matumizi ya baadaye. Hapa kulipa inamaanisha adhabu kwa ajili ya dhambi. KTN: "Mungu hutunza kumbukumbu ya dhambi za mtu, kisha huwaadhibu watoto wa mtu huyo kwa matendo yake maovu"
|
||
|
|
||
|
# alipe yeye mwenyewe
|
||
|
|
||
|
Ayubu anaanza kutoa mawazo yake. KTN: " Lakini mimi nasema, alipe yeye mwenyewe"
|
||
|
|
||
|
# Macho yake mwenyewe yaone
|
||
|
|
||
|
"Macho" ni rejea kwa mtu.KTN: "aweze kuona yeye mwenyewe"
|
||
|
|
||
|
# anywe ghadhabu Mwenyezi
|
||
|
|
||
|
Ghadhabu ya Mungu inasema kana kwamba ni kinywaji ambacho mtu anaweza kuonja. Ayubu anataka waovu wapate adhabu ya Mungu.
|
||
|
|
||
|
# Kwani anajali nini kuhusu familia yake baada ya idadi ya miezi yake kuondolewa?
|
||
|
|
||
|
Ayubu anatumia swali kuonesha kuwa kuwaadhibu watoto wa mtu mwovu haina nguvu.KTN: "Kwani mtu mwovu hajali kuhusu familia yake baada ya kufa!"
|
||
|
|
||
|
# idadi ya miezi yake kuondolewa
|
||
|
|
||
|
hii ni namna ya staha kusema anapofariki.
|
||
|
|
||
|
# idadi ya miezi yake
|
||
|
|
||
|
Hii inarejea urefu wa miaka ya maisha yake.
|
||
|
|