sw_ulb/39-MAL.usfm

104 lines
9.1 KiB
Plaintext
Raw Permalink Blame History

This file contains ambiguous Unicode characters

This file contains Unicode characters that might be confused with other characters. If you think that this is intentional, you can safely ignore this warning. Use the Escape button to reveal them.

\id MAL
\ide UTF-8
\h Malaki
\toc1 Malaki
\toc2 Malaki
\toc3 mal
\mt Malaki
\c 1
\cl Sura 1
\p
\v 1 Tamko la neno la Bwana kwa Israeli kwa mkono wa Malaki.
\p
\v 2 “Nilikupenda, “asema Bwana. Lakini unasema, “kwa jinsi gani ulinipenda?” Esau siyo ndugu yake Yakobo?” asema Bwana. “Na bado nampenda Yakobo,
\v 3 lakini nimemchukia Esau. Nimeifanya milima yake kuwa ukiwa, na nimepafanya urithi wake kuwa makao ya mbweha wa jangwani.”
\p
\v 4 Kama Edomu husema, “Tumepigwa, lakini tutarudi na kujenga palipoharibiwa; “Bwana wa Majeshi asama hivi, “Watajenga lakini nitaiangusha chini; na wanaume watawaita Nchi ya uovu, na Watu ambao Mungu ana hasira nao milele.”
\v 5 Kwa macho yenu mtaona hili, na mtasema, “Bwana ni mkuu mbele ya mipaka ya Israel.”
\p
\v 6 Mtoto amtii baba yake, na mtumwa amtii bwana wake. Ikiwa mimi, ni baba, iko wapi heshima yangu? Na kama mimi ni bwana, iko wapi heshima yangu? Bwana wa majeshi asema hivi kwenu, makuhani, mnaodharau jina langu. Lakini mnasema, tumeridharauje jina lako?
\pi
\v 7 Kwa kutoa mikate iliyonajisi madhabahuni kwangu. Na mnasema kuwa, Tumekudharau kwa namna gani? Kwa kusema hivyo meza ya Bwana imedharauliwa.
\pi
\v 8 Mkitoa sadaka ya wanyama vipofu, hiyo siyo dhambi? Na kama mkitoa vilema na wagonjwa, hiyo siyo dhambi? Pelekeni hili kwa liwali; atawakubali au atainua nyuso zetu?” asema Bwana wa Majeshi.
\p
\v 9 Na sasa, mnajaribu kutafuta neema ya Mungu, ili kwamba awe mwema kwetu. “Na aina gani ya sadaka kwa sehemu yenu, ataziinua nyuso zenu? Asema Bwana wa Majeshi.
\p
\v 10 Kama kungekuwa na mtu ambaye angefunga lango la Hekalu, ili kwamba kusiwepo na moto madhabahuni bure! Lakini sina radhi na ninyi, “asema Bwana wa majeshi, “na sitaikubali sadaka yeyote kutoka katika mikono yenu.
\v 11 Kutoka mawio ya jua mpaka machweo jina langu litakuwa kuu katikati ya mataifa; katika kila sehemu uvumba utatolewa katika jina langu, na pia sadaka safi. Kwa sababu jina langu litakuwa kuu sana katikati ya mataifa,” asema Bwana wa majeshi.
\p
\v 12 “Lakini ninyi mnachafua mnaposema meza ya Bwana mnainajisi, na matunda yake, na chakula chake kudharaurika.”
\pi
\v 13 Na ninyi pia mwasema, “jambo hili limetuchosha, nanyi mnalidharau,” asema Bwana wa majeshi. “Mmerudisha kilichokuwa kimechukuliwa na wanyama wa mwitu au vilema au walio wagonjwa; na ndicho mnaleta kuwa sadaka zenu! Je naweza kuikubali hii mikononi mwenu?” asema Bwana.
\p
\v 14 Alaaniwe aliye mdanganyifu, ambaye anaye mnyama dume katika kundi lake na akaahidi kunitolea, lakini bado anatoa kwangu, mimi Bwana, ambayo ni kiujanja ujanja; kwa kuwa mimi ni mfalme mkuu,” asema Bwana wa Majeshi, “na jina langu litaogopwa katika mataifa.”
\c 2
\cl Sura 2
\p
\v 1 “Sasa, ninyi makuhani, amri hii ni kwa ajili yenu.
\v 2 Kama hamtasikiliza, na kama hamtalichukua hili mioyoni mwenu na kunipa utukufu kwa jina langu,” asema Bwana wa Majeshi, Kisha nitatuma laana kwenu, na nitalaani baraka zenu. Kiukweli, nilishawalaani tayari, kwa sababu hujaweka sheria zangu moyoni.
\v 3 Tazama, nitakikemea kizazi chako, na nitapaka mavi juu ya uso wako, mavi ya dhabihu zenu, na mtachukuliwa pamoja nayo.
\p
\v 4 Na mtajua kwamba nimetuma hii sheria kwenu, kwamba agano langu litakuwa ni juu yangu na Lawi,” asema Bwana wa Majeshi.
\v 5 Agano langu na yeye lilikuwa agano la uhai na amani, na nilimpa vitu hivi kama njia ya kuniheshimu. Aliniheshima na alisimama akawa na hofu kwa jina langu.
\v 6 Mafundisho ya kweli yalikuwa kwenye kinywa chake, na uovu haukupatikana kinywani mwake. Alitembea na mimi kwa amani na unyofu, na aliwarudisha wengi kutoka dhambini.
\p
\v 7 Kwa sababu midomo ya makuhani huhifadhi maarifa, na watu watatafuta maagizo kutoka kwenye kichwa chake, kwa sababu ni mjumbe wa Bwana wa Majeshi.
\p
\v 8 Lakini umepita mbali na njia ya kweli. Umesababisha wengi kuwa na mashaka ya kutii sheria. Umeliharibu agano la Lawi,” asema Bwana wa Majeshi.
\v 9 Kwa hiyo nimewafanya ninyi nanyi kudharauliwa mbele ya watu, kwa sababu hamkutunza njia zangu, lakini badala yake mnapendelea katika maagizo yenu.
\p
\v 10 Sisi sote hatuna baba mmoja? Siyo Mungu yule mmoja aliyetuumba sote? Kwa nini tunafanyiana hila kila mtu na ndugu yake, mnaliharibu agano la baba zetu?
\p
\v 11 Yuda amefanya hila na ameona kinyaa kwa vitu vilivyowekwa katika Israeli na Yerusalem. Yuda amenajisi mahali patakatifu pa Bwana ambapo anapapenda, na ameoa binti wa miungu migeni.
\v 12 Mungu akukatilie mbali kutoka kwenye hema ya Yakobo na uzao wa mtu aliyefanya haya, hata yule anayeleta sadaka kwa Bwana wa Majeshi.
\p
\v 13 Na wewe pia fanya hivyo. Unafunika madhabahu ya Bwana kwa machozi, kwa kilio na kuugua, kwa sababu hatakubali sadaka na kuzipokea kutoka mikononi mwako.
\v 14 Lakini wasema, ni kwa sababu gani?” Kwa sababu Bwana amekuwa shahidi kati yako wewe na mke wako wa ujana wako, kinyume chake umekuwa si mwaminifu, ingawa yeye ni mwenzako na mke wa agano lako.
\p
\v 15 Je yeye hakuwafanya kuwa mmoja, hata kwa sehemu ya roho yake? Sasa ni kwa nini aliwafanya ninyi kuwa mmoja? Kwa sababu alikuwa anategemea kupata watoto wacha Mungu. Kwa hiyo jiepushe mwenyewe ndani ya moyo wako, na asiwepo mtu asiye mwaminifu kwa mke wa ujana wake.
\p
\v 16 “Nakuchukia kuachana,” asema Bwana, Mungu wa Israel, “afunikizaye nguo yake kwa udhalimu,” asema Bwana wa Majeshi. “Kwa hiyo jilinde ewe mwenyewe ndani ya roho yako na usiwe mtu asiye mwaminifu.”
\p
\v 17 Mmemchosha Bwana na maneno. Lakini mwasema, “Tumekuchoshaje?” Kwa kusema Kila mmoja aliyefanya uovu ni mzuri kwa upande wa Bwana, na anafuraha nao;” au “Yuko wapi Mungu wa Haki?”
\c 3
\cl Sura 3
\p
\v 1 Tazama, namtuma mjumbe wangu, atakaye andaa njia mbele yangu. Na Bwana, ambaye mnamtafuta, atakuja ghafla katika hekalu lake; na mjumbe wa agano, ambaye katika yeye mnafurahi, tazama anakuja.” Asema.” Bwana wa Majeshi.
\p
\v 2 Nani nani atakeye vumilia siku ya kuja kwake? Ni nani atasimama akishatokea? Yeye ni kama mtu asafishaye kwa moto na kama sabuni ya kufulia.
\v 3 Atakaa na kutawala kama msafishaji wa fedha, na atawasafisha wana wa Lawi. Na atawafanya wawe safi kama dhahabu na fedha, na wataleta sadaka za haki kwa Bwana.
\v 4 Na sadaka ya Yuda na Yerusalem itampendeza Bwana, kama siku za kale, na miaka ya zamani.
\p
\v 5 Kisha nitapita karibu na ninyi kuwahukumu. Na nitakuwa shahidi mwepesi dhidi ya wachawi, wazinzi, mashahidi wa uongo, na kinyume cha wale wanao onea wafanya kazi katika mizigo yake, wanao onea wajane na yatima, na anayemfukuza mgeni kutoka kwenye haki yake, na kwa wale wasionitii mimi,” asema Bwana wa majeshi.
\pi
\v 6 Mimi Bwana, sibadiliki; pia ninyi, watu wa Yakobo, hamkutumia.
\v 7 Toka siku za baba zenu mmegeukia mbali na amri zangu na hamkuzitunza. Nigeukieni, nami nitawarudia ninyi,”,” asema Bwana wa majeshi. Lakini mwasema, tutakurudiaje?
\pi
\v 8 Mwanadamu anaweza kumwibia Mungu? Mnaniibia mimi, lakini mwasema, Tumekuibiaje? kwa zaka na sadaka.
\v 9 Mmelaaniwa kwa laana, kwa kuniibia mimi, taifa lote hili.
\v 10 Leteni zaka kamili katika ghalani, ili kwamba kiwemo chakula katika nyumba yangu. Na mnijaribu kwa hili,” asema Bwana wa Majeshi. “Kama sitawafungulia madirisha ya mbinguni na kuwamwagia baraka juu yenu, ili kwamba hakutakuwa na sehemu ya kutosha kuzipokea.
\v 11 Nitamkemea mharibifu kwako, kwamba asiharibu mavuno yenu ya nchi yenu; mizazibu yenu katika shamba haitapukutisha kabla ya wakati wake,”,” asema Bwana wa Majeshi.
\v 12 Mataifa yote watakuita mbarikiwa; kwa ajili yako itakuwa ni nchi ya furaha,” asema Bwana wa Majeshi.
\pi
\v 13 “Maneno yenu yamekuwa magumu kinyume changu,” asema Bwana. “Lakini mwasema, Tumesema nini kinyume chako?
\p
\v 14 Mmesema, Hakuna maana kumtumikia Mungu. Kuna faida ya namna gani kutunza maagizo yake au kutembea huku mkiomboleza mbele za Bwana wa Majeshi?
\v 15 Na sasa tunamwita mwenye kiburi mbarikiwa. Wahalifu si kufanikiwa tu, bali kumjaribu Mungu na kumuepuka.”
\p
\v 16 Kisha wale wanao muheshimu Bwana walisemezana mmoja baada ya mwingine; Bwana yuko makini kutusikiliza, na kitabu cha kumbukumbu kiliandikwa mbele zake kwa ajili ya wale walio mwogopa Bwana na kuliheshimu jina lake.
\p
\v 17 “Watakuwa wangu,” asema Bwana wa majeshi,” hazina zangu, katika siku nitakayotenda; nitawapenda, kama mtu anavyompenda mwanawe anayemhudumia.
\v 18 Kisha zaidi sana nitatofautisha kati ya wenye haki na waovu, kati ya anayemwabudu Mungu na asiyemwabudu yeye.
\c 4
\cl Sura 4
\p
\v 1 Tazama, siku inakuja, inawaka kama tanuru, ambayo wote wenye kiburi na wahalifu watakuwa mabua. Siku inakuja itawachoma,” asema Bwana wa Majeshi, “siku hiyo itaondoa mzizi au shina.
\v 2 Lakini kwenu mnaoliogopa jina langu, jua la haki litawaangazia na uponyaji katika mbawa zake. Mtarukaruka kama ndama zizini.
\v 3 Na waovu wote mtawakanyaga chini, watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu siku hiyo nitatenda,” asema Bwana wa Majeshi.
\p
\v 4 Kumbukeni kutii sheria za mtumishi wangu Musa, amri na sheria nilizomwamuru huko Horebu, kwa Israeli wote.
\p
\v 5 Tazama, nitamtuma Eliya nabii mbele yenu kabla ya siku kuu na yenye kutisha ya kuja kwa Bwana.
\v 6 Atarudisha moyo wa baba kwa watoto, na mioyo ya watoto kwa baba zao; ili kwamba nisije nikaiangamiza nchi kwa uharibifu wote.”