# Sentensi unganishi Baada ya kumponya mtu aliyemilikiwa na pepo katika mji wa Gerasenes, Yesu na wanafunzi wake wanarudi kupitia ziwa Kaperinaumu ambapo mmoja wa watawala wa sinagogi anamuuliza Yesu kumponya binti yake. # upande mwingine Inaweza kuwa msaada kuongoza taarifa kwa maneno haya. "upande wa pili wa bahari" # kando mwa bahari "ufukoni mwa bahari" au "katika ufuko" # bahari Hili ni bahari la Galilaya. # Yairo Hili ni jina la mwanaume. # Kwa hiyo alienda kwake "Hivyo Yesu alienda pamoja na Yairo." Wanafunzi wa Yesu walienda pia naye. "Hivyo Yesu na wanafunzi walienda na Yairo" # weka mikono yako "Kuweka mikono" urejea kwa nabii au mwalimu kuweka mkono wake kwa mtu na kugawa aidha uponyaji au baraka. Katika jambo hili, Yairo anamuomba Yesu kumponya binti yake. # kwamba afanywe mzima na aishi Hii inaweza kusemwa katika kauli tendaji. "na mponye na kumfanya hai" # na walimzonga karibu wakimzunguka. Hii inamaanisha umati walimzunguka Yesu na kujisonga wenyewe kuwa karibu na Yesu.