\v 1 Paulo, mtume wa Kristo Yesu kwa mapenzi ya Mungu, na Timotheo ndugu yetu,
\v 2 kwa watu watakatifu wa Mungu na ndugu waaminifu katika Kristo walioko Kolosai. Neema iwe kwenu, na amani kutoka kwa Mungu Baba yetu.
\p
\v 3 Tunatoa shukrani kwa Mungu, Baba wa Bwana wetu Yesu Kristo, na tunawaombea kila mara.
\v 4 Tumesikia imani yenu katika Yesu Kristo na upendo mlionao kwa watu wote watakatifu wa Mungu,
\v 5 kwa sababu ya taraja la uhakika lililohifadhiwa mbinguni kwa ajili yenuMlisikia kuhusu taraja hiyo ya uhakika katika neno la ukweli, injili
\v 6 ambayo imekuja kwenu. Na kwa njia hiyo hiyo, Injili hii inazaa tunda na inaenea ulimwenguni koteImekuwa ikifanya hivi ndani yenu tangu siku mlipoisikia na kufahamu neema ya Mungu katika kweli.
\v 7 Hii ndiyo injili kama mlivyojifunza kutoka kwa Epafra, mtumishi mwenzetuambaye ni mtumishi mwaminifu wa Kristo kwa ajili yetu.
\v 9 Kwa sababu ya upendo huu, tangu siku tuliposikia hivi, hatujakoma kuwaombea. Tumekuwa tukiomba kwamba mtajazwa na maarifa ya mapenzi yake katika hekima yote na ufahamu wa kiroho,
\v 10 Tumekuwa tukiomba kwamba mtatembea kwa ustahimilivu wa bwana katika njia zipendezazo Bwana. Tumekua tukiomba mtazaa tunda katika kila tendo jema na kwamba mtakua katika maarifa ya Mungu.
\v 11 Tunaomba muweze kutiwa nguvu katika kila uwezo kulingana na nguvu za utukufu wakekatika uvumilivu na ustahimilivu wote.
\v 12 Tunaomba kwamba kwa furahamtatoa shukrani kwa Baba aliyewafanya ninyi mweze kuwa na sehemu katika urithi wa waumini katika nuru.
\p
\v 13 Ametuokoa kutoka katika utawala wa giza, akatuhamishia katika ufalme wa Mwana wake mpendwa.
\v 14 Katika mwanae tuna ukombozi na msamaha wa dhambi.
\v 15 Mwana ni mfano wa Mungu asiyeonekana, mzaliwa wa kwanza wa uumbaji wote.
\v 16 Kwa kuwa kwa yeye vitu vyote viliumbwa, vile vilivyoko mbinguni na vilivyoko duniani, vitu vinavyoonekana na visivyoonekana. Ikiwa ni vya enzi au mamlaka au utawala au wenye nguvu, vitu vyote viliumbwa na yeye na kwa ajili yake.
\v 18 Na yeye ndiye kichwa cha mwili yaani kanisa, yeye ni mwanzo, na mzaliwa wa kwanza kutoka miongoni mwa wafu, hivyo, ana nafasi ya kwanza miongoni mwa vitu vyote.
\v 19 Kwa kuwa Mungu alipendezwa kwamba utimilifu wake wote uishi ndani yake,
\v 20 na kupatanisha vitu vyote kwake kwa njia ya Mwanawe. Mungu alifanya amani kupitia damu ya msalaba wake. Akapatanisha vitu vyote kwake mwenyewe, ikiwa ni vitu vya duniani au vitu vya mbinguni.
\p
\v 21 Nanyi pia, kwa wakati mmoja, mlikuwa mmetengwa na Mungu na mlikua maadui katika akili na matendo maovu.
\v 22 Lakini sasa amewapatanisha ninyi kwa mwili wake kupitia kifo. Alifanya hivi ili kuwaleta ninyi watakatifu, wasio na lawama na bila dosari mbele yake,
\v 23 kama mkiendelea katika imani, mliyoimarishwa na kuwa thabiti, pasipo kuondoshwa kutoka kwenye taraja la ujasiri la injili mliyoisikia. Hii ndiyo injili ambayo ilihubiriwa kwa kila kiumbe chini ya mbingu. Hii ndiyo injili ambayo kwayo mimi, Paulo, nimekuwa mtumishi.
\p
\v 24 Sasa nayafurahia mateso yangu kwa ajili yenu. Nami natimiliza katika mwili wangu kinachopungua kwa mateso ya Kristo kwa ajili ya mwili wake, ambao ni kanisa.
\v 25 Mimi ni mtumishi wa kanisa hili, sawasawa na wajibu niliopewa kutoka kwa Mungu kwa ajili yenu, kulitimiza neno la Mungu.
\v 26 Huu ni ukweli wa siri iliyofichwa kwa miaka mingi na kwa vizazi. Lakini sasa imefunuliwa kwa wote waaminio katika yeye.
\v 27 Ni kwa wale ambao Mungu alitaka kufunua ulivyo utajiri wa utukufu wa siri ya ukweli miongoni mwa Mataifa, Ni kwamba Kristo yumo ndani yenu, ujasiri wa utukufu ujao.
\v 28 Huyu ndiye tunayemtangaza. Tunamwonya kila mtu, na kumfundisha kila mtukwa hekima yote, ili kwamba tumlete kila mtu mkamilifu katika Kristo.
\v 29 Kwa ajili hii, mimi najibiidisha na kujitahidi kulingana na nguvu yake ifanyayo kazi ndani yangu katika uweza.
\v 1 Kwa kuwa nataka mfahamu jinsi ambavyo nimekuwa na taabu nyingi kwa ajili yenu, kwa wote walioko Laodikia, na kwa wote ambao hawajauona uso wangu katika mwili.
\v 2 Nafanya kazi ili mioyo yao ifarijiwe, kwa kuletwa pamoja katika upendo na katika utajiri wote wa wingi wa uhakika kamili na maarifa, katika kuijua siri ya kweli ya Mungu, ambaye ni Kristo.
\v 5 Na ingawa sipo pamoja nanyi katika mwili, lakini nipo nanyi katika roho. Ninafurahi kuona utaratibu wenu mzuri na nguvu ya imani yenu katika Kristo.
\v 6 Kama mlivyompokea Kristo Bwana, tembeeni katika yeye.
\v 7 Mwe na mzizi ndani yake, mjengwe katika yeye, mwimarishwe katika imani kama tu mlivyofundishwa, na kufungwa katika shukrani nyingi.
\p
\v 8 Angalieni ya kwamba mtu yeyote asiwanase kwa falsafa na maneno matupu ya udanganyifu kulingana na mapokeo ya wanadamu, kulingana na kanuni za kidunia, na sio kulingana na Kristo.
\v 18 Mtu awaye yeyote asinyang'anywe tuzo yake kwa kutamani unyenyekevu na kuabudu malaika. Mtu wa jinsi hiyo huingia katika mambo aliyoyaona na kushawishiwa na mawazo yake ya kimwili.
\v 19 Yeye hakishikilii kichwa. Ni kutoka katika kichwa kwamba mwili wote kupitia viungo vyake na mifupa huungwa na kushikamanishwa kwa pamoja; na hukua kwa ukuaji utolewao na Mungu.
\v 9 Msidanganyane ninyi kwa ninyi, kwa kuwa mmeuvua utu wenu wa kale na matendo yake.
\v 10 Mmevaa utu upya, unaofanywa upya katika maarifa sawasawa na mfano wa yule aliyeuumba.
\v 11 Katika maarifa haya, hakuna Myunani wala Myahudi, kutahiriwa wala kutokutahiriwa, msomi, asiye msomi, mtumwa, mtu huru, bali Kristo ni mambo yote katika yote.
\p
\v 12 Kama wateule wa Mungu, watakatifu na wapendwao, jivikeni utu wema, ukarimu, unyenyekevu, upole na uvumilivu.
\v 13 Chukulianeni ninyi kwa ninyi. Hurumianeni kila mtu na mwenzake. Kama mtu analalamiko dhidi ya mwingine, amsamehe kwa jinsi ileile ambayo Bwana alivyo wasamehe ninyi.
\v 15 Amani ya Kristo itawale mioyoni mwenu. Ilikuwa ni kwa ajili ya amani hii mliitiwa katika mwili mmoja. Iweni na shukrani.
\v 16 Na Neno la Kristo likae ndani yenu kwa wingi. Kwa hekima yote, fundishaneni na kushauriana ninyi kwa ninyi kwa Zaburi katika hekima yote, mkimwimbia saburi, na nyimbo, na tenzi za rohoni. Imbeni kwa shukrani mioyoni mwenu kwa Mungu.
\p
\v 17 Na chochote mfanyacho katika maneno au katika matendo, fanyeni yote katika jina la Bwana Yesu. Mpeni shukrani Mungu baba kupitia Yeye.
\p
\v 18 Wake, wanyenyekeeni waume zenu, kama ipendezavyo katika Bwana.
\v 19 Nanyi waume, wapendeni wake zenu, na msiwe wakali dhidi yao.
\p
\v 20 Watoto, watiini wazazi wenu katika mambo yote, maana ndivyo impendezavyo Bwana.
\v 22 Watumwa, watiini mabwana zenu katika mwili kwa mambo yote, sio kwa huduma ya macho kama wapendezao watu tu, bali kwa moyo wa kweli. Mcheni Mungu.
\v 23 Chochote mfanyacho, fanyeni kutoka nafsini mwenu kama kwa Bwana na si kama kwa wanadamu.
\v 24 Mnajua ya kwamba mtapokea ujira wa urithi kutoka kwa Bwana. Ni Kristo Bwana mnayemtumikia.
\v 2 Endeleeni kuwa thabiti katika maombi. Kaeni macho katika hilo kwa shukrani.
\v 3 Mkituombea pamoja pia, ili kwamba Mungu afungue mlango kwa ajili ya neno, kunena siri ya ukweli ya Kristo. Kwa sababu ya hili nimefungwa minyororo.
\v 4 Ombeni kwamba niweze kulweka wazi kama inavyonipasa kusema.
\p
\v 5 Enenda kwa hekima kwa wale walioko nje, na muukomboe wakati.
\v 10 Aristarko, mfungwa mwenzangu, anawasalimu, pia na Marko binamu yake na Barnaba mliyepokea utaratibu kutoka kwake, “kama akija kwenu, mpokeeni,”
\v 11 Na pia Yesu aitwaye Yusto. Hawa peke yao wa tohara ni watendakazi wenzangu kwa ajili ya ufalme wa Mungu. Wamekuwa ni faraja kwangu.
\v 12 Epafra anawasalimu. Yeye ni mmoja wenu na mtumwa wa Kristo Yesu. Yeye hujitahidi siku zote katika maombi kwa ajili yenu ili kwamba mweze kusimama kwa ukamilifu na kuhakikishwa kikamilifu katika mapenzi yote ya Mungu.
\v 13 Kwa kuwa ninamshuhudia, kwamba anafanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa hao walioko Laodekia, na kwa hao walioko Hierapoli.