1.1 KiB
Sentensi unganishi.
Yesu anaendelea kuwaelekeza wanafunzi wake kuhusu kutohofia dhiki itakayowakabili.
Yeye atakaye
Neno "yeye" linamaanisha mtu yeyote. "yeyote" au "yeyote ambaye" au " ambaye"
atakayewakaribisha
Inamaanisha kumkaribisha mtu kama mgeni
Wa
Kiwakilishi "wa" kinamaanisha mitume kumi na wawili ambao Yesu anawaaambia.
ananikaribisha mimi
Yesu anamaanisha ni sawa na kumkaribisha yeye. "ni kama ananikaribisha mimi" au "ni kama vile alikuwa ananikaribisha mimi"
kumkaribisha yeye aliyenituma
Hii inamaanisha wakati mtu anamkaribisha Yesu ni sawa na kumkaribisha Mungu. "ni kama vile kumkaribisha Mungu aliyenituma"
Kwa sababu ni nabii
Hapa kiwakilishi cha "ni" kinamaanisha mtu anayekaribishwa.
thawabu ya nabii
Hii inamaanisha zawadi ambayo Mungu anampa nabii. wala siyo zawadi ambayo nabii anampatia mtu mwingine.
mtu wa haki
Hapa "wa" haimaanishi mtu anayekaribisha. Inamaaanisha mtu anayekaribishwa.
thawabu ya mtu wa haki
Hii inamaanisha zawadi ambayo Mungu humpa mtu wa haki, siyo zawadi ambayo mtu wa haki humpatia mtu mwingine.