# Taarifa ya Jumla: Usambamba ni kawaida katika mashairi ya Kiebrania. # Taarifa ya Jumla: Zaburi hii ni ombi kwa ajili ya msaada. # Kwa mwanamuziki mkuu "Hii ni kwa kiongozi wa muziki kutumia katika kuabudu" # kwenye vyombo vya nyuzi "watu wanapaswa kucheza vyombo vya nyuzi na wimbo huu" # Maschili Hii inaweza kumaanisha mtindo wa muziki. # Wafizi Watu kutoka mji wa Zifu katika milima ya Yuda, kusini mashariki mwa Hebroni. # Kwani Daudi hajifichi pamoja na sisi? Swali hili linatumika kuonesha kuwa hili ni jambo muhimu ambalo Sauli anapaswa kujua. "Daudi anajificha na sisi." # Niokoe, Mungu, kwa jina lako Hapa jina la Mungu linaashiria tabia yake. Inaweza kumaanisha zaidi uwezo wake au haki yake. "niokoe, Mungu, kwa uwezo wako" # nihukumu katika uwezo wako Kumhukumu Daudi hapa inaashiria kuwaonesha watu kuwa Daudi hana hatia. Mungu anapotumia nguvu zake kumwokoa Daudi, watu watajua kuwa Mungu amemhukumu na hana hatia. "Kwa uwezo wako, waoneshe watu kuwa sina hatia" au "Waoneshe watu kuwa sina hatia kwa kutumia nguvu zako kuniokoa" # yape masikio maneno ya Kumpa mtu masikio inaashiria kumsikiliza. "sikiliza maneno yangu" # maneno ya mdomo wangu Msemo huu unamaanisha kile alichosema mnenaji. "maneno yangu" au "ninachosema kwako" # wameinuka dhidi yangu Kuinuka dhidi ya mtu inaashiria kujiandaa kumshambulia au kumshambulia kabisa. "wamejiandaa kunishambulia" au "wananishambulia" # watu wasio na huruma "wanaume wasio na huruma" # wametafuta maisha yangu Kutafuta maisha ya mtu inamaanisha kujaribu kumuua. "wamejaribu kuniua" au "wanataka kuniua" # hawajamuweka Mungu mbele yao Kumweka Mungu mbele yao inaashiria kuwa makini na Mungu. "hawamzingatii Mungu" au "hawamjali Mungu"