# Anawatiisha watu chini yetu na mataifa chini ya miguu yetu. Misemo hii miwili ina usambamba na inamaanisha kuwa Mungu aliwezesha Israeli kuwashinda adui zake. # Anawatiisha Kushinda na kuweka chini ya mamlaka ya mwingine # chini yetu ... chini ya miguu yetu Mwandishi anazungumzia kuyashinda mataifa mengine kana kwamba ilikuwa kuyaweka mataifa hayo chini ya miguu yao. # Anatuchagulia urithi wetu Mwandishi anazungumzia nchi ya Israeli kana kwamba ilikuwa ni urithi ambao Mungu aliwapa watu kama mali ya milele. "Anachagua nchi hii kama urithi wetu" # utukufu wa Yakobo Hapa neno "utukufu" inmaanisha chanzo cha majivuno na linaashiria nchi ambayo Mungu amewapa watu wake kama urithi. "nchi ambayo Yakobo anajivunia" # Yakobo aliyempenda Neno "Yakobo" linaashiria taifa la Israeli. # Mungu ameenda juu kwa shangwe Mwandishi anamzungumzia Mungu kuyashinda mataifa kana kwamba Mungu alikuwa mfalme anaye panda kwenye kiti chake cha enzi, kilicho kuwa hekaluni. "Mungu ameenda juu kwenye hekalu wakati watu wakipiga shangwe" (UDB) au "Mungu amepanda kwenye kiti chake cha enzi wakati watu wakipiga shagngwe" # Yahwe kwa sauti ya tarumbeta Msemo huu uko sambamba na msemo uliopita. Kitenzi kinaweza kuwekwa kuweka wazi. "Yahwe ameenda juu wakati watu wakipuliza tarumbeta"