# Bora kidogo alichonacho mwenye haki kuliko kingi cha watu waovu wengi Hapa mstari wa pili ni tofauti na wa kwanza. "Ni bora kuwa mwenye haki, hata kama inamaanisha utakuwa maskini, kuliko kuwa mwovu na utajiri mkubwa" # Bora kidogo alichonacho mwenye haki "Ni bora kuwa mwenye haki, hata kama inamaanisha utakuwa maskini" # kidogo Hii inamaanisha kuwa na mali kidogo. # mwenye haki Hii inamaanisha mtu mwenye haki. "mtu mwenye haki ana" # kingi Hii inamaanisha utajiri wa watu waovu. # Kwa kuwa mikono ya watu waovu itavunjwa Hapa "mikono" inawakilisha nguvu ya watu waovu. Kuvunja mikono yao inawakilisha kuwanyanganya nguvu yao. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "Kwa kuwa Yahwe ataondoa uwezo wa watu waovu"