# Taarifa ya Jumla: Sasa mwandishi anaeleza jinsi Mungu ni kama mtu anayemkaribisha mgeni nyumbani kwake na kumlinda. # Unaandaa Meza inaashiria karamu kwa sababu watu huweka chakula chote mezani. # mbele ya adui zangu Maana hapa ni kwamba mwandishi hana wasiwasi kuhusu adui zake kwa sababu yeye ni mgeni wa heshima wa Bwana na kwa hiyo analindwa na madhara. "licha ya uwepo wa adui zangu" # unatia kichwa changu mafuta Watu wakati mwingine huweka mafuta kwenye vichwa vya wageni wao ili kuwapa heshima. # kikombe changu kinamwagikia Hapa kikombe cha divai kinachotiririka kinaashiria baraka nyingi. "Unajaza kikombe changu sana hadi kinamwagikia" au "unanipa baraka nyingi"