# Maelezo ya Jumla Yahwe anaendelea kuzungumza na watu wa Yerusalemu. # Katika hasira iliyofurika Yahwe kuwa na hasira sana inazungumziwa kana kwamba hasira yake ilikuwa mafuriko ambayo yanawazidi watu. "Nilipokuwa na hasira sana" # Nimeficha uso wangu kutoka kwako Hapa "kuficha uso wangu" ni lahaja ambayo ina maana ya Mungu kutelekeza watu wake na kuwaacha wateseke. "Nilikutelekeza" # lakini kwa agano la uaminifu la milele Nomino dhahania "uaminifu" inaweza kuwekwa kama "mwaminifu". "lakini kwa sababu mimi ni mwaminifu siku zote kwa agano langu na wewe" au "lakinii kwa sababu mimi ni mwaminifu kufanya kile nilichoahidi kufanya" # anasema Yahwe, ambaye anakuokoa wewe Hapa Yahwe anazungumzia juu yake katiika mtu wa tatu. Inaweza kuwekwa katika mtu wa kwanza. "hivi ndivyo mimi, Yahwe, mkombozi wako, nasema kwako"