# Sentensi unganishi Viongozi wa dini walimkamata Petro na Yohana baada ya Petro kumponya yule mtu aliyezaliwa kiwete. # wakaja kwao "waliwasogelea" au "walikuja kwao" # Walikuwa wameudhika sana Walikuwa na hasira. Masadukayo kwa upekee wao wangekuwa na hasira kwa Petro na Yohana kwasababu hawakuamini ufufuo. # walikuwa wanawafundisha watu kuhusu Yesu na kutangaza juu ya kufufuka kwake kutoka kwa wafu Petro na Yohana walikuwa wakisema Mungu angewainua watu kutoka mautini sawa na vile Yesu alivyoinuliwa kutoka miongoni mwa wafu. Petro anazungumzia ufufuo wa Yesu na ufufuo wa watu wote kwa ujumla. # Waliwakamata Makuhani na mlinzi wa hekalu pamoja na Masadukayo waliwakamata Petro na Yohana. # Kwavile ilikuwa jioni sasa Ilikuwa tendo la kawaida kutowahoji watu wakati wa usiku. # na idadi ya wanaume waliokuwa wameamini Hii inamanisha kwa idadi ya wanaume tu, wanawake na watoto walioamini hawakuhesabiwa. # Walikuwa yapata elfu tano "walikuwa kama elfu tano" au "iliongezeka hadi elfu tano"