# Taarifa ya Jumla: Hii ni sehemu ya maono ya Yohana ifuatayo. Hapa anaelezea furaha ya mbinguni juu ya kuanguka kwa kahaba mkuu, ambaye ni mji wa Babeli. # nilisikia Hapa aliyesikia ni Yohana. # Haleluya Neno hili linamaana "Msifu Mungu" au "Tumsifu Mungu." # kahaba mkuu Hapa Yohana anamaanisha mji wa Babeli ambao watu wake waouvu wanawatawala watu wote duniani na kuwaongoza kuabudu miungu ya uuongo. Anawazungumzia watu waovu wa Babeli kana kwamba ni kahaba mkuu. # aliyeiharibu nchi Hapa "nchi" ni njia nyingine ya kusema wakazi. "waliwaharibu watu wa duniani" # damu ya watumishi wake Hapa "damu" ni njia nyingine ya kuwakilisha mauaji. "kuwaua watumishi wake" # yeye mwenyewe Hii inamaanisha Babeli. Kurudiwa kwa haya maneno ni kwa ajili ya kuongeza msisitizo.