# tutafurahi katika ushindi wako Hapa watakaofurahi ni watu. Watufurahi katika ushindi wa mfalme. # katika jina la Mungu wetu Hapa "jina" linamaanisha heshima na sifa. "kwa heshima ya Mungu" au "kwa sifa ya Mungu wetu" # tutanyanyua bendera "tutanyanyua mabango" # akupe maombi yako yote "kukupa kila kitu unachomuomba" # Sasa Neno hili linatumika kuweka mapumziko katika zaburi. Inahama kutoka kwa watu kuzungumza hadi kwa mfalme kuzungumza. # Ninajua Anayejua inawezekana ni mfalme katika kipengele hiki. # mtiwa mafuta wake ... atamjibu ... atamuokoa Mfalme anajizumzia mwenyewe katika hali ya mtu wa tatu. Hii inaweza kuelezwa katika hali ya mtu wa kwanza. "mimi, mtiwa mafuta wake ... nijibu .. niokoe" # kutoka mbingu yake takatifu Mungu anaishi mbinguni pamoja na kwenye hekalu Yerusalemu. # kwa nguvu ya mkono wake wa kuume unaoweza kumwokoa Mkono wa kuume wa Mungu unaashiria nguvu yake kumwokoa mfalme. "kwa nguvu yake kubwa atamwokoa"