# Sentensi unganishi Yesu anaanza kwa kufundisha jinsi alivyokuja kuitimiliza sheria ya agano la kale # manabii Hii inamaanisha kile walichoandika manabii katika maandiko. # kweli nawaambieni "Nawaambia ukweli" Kirai hiki kinaongeza nguvu juu ya kile Yesu atakachosema baadaye. # mpaka mbingu na dunia zote zipite Hapa "mbingu" na "dunia" humaanisha ulimwengu wote. "Kama vile mbingu zidumuvyo" # hapana yodi moja wala nukta moja "hapana hata ile herufi ndogo iliyoandikwa au sehemu ndogo ya herufi. Hii ni sitiari inayomaanisha kitu fulani katika maandiko kinachoweza kuonekana kuwa si cha muhimu. "wala sheria zinazoonekana kuwa si za muhimu # kila kitu kitakapokuwa kimetimizwa Hiki kinaweza kuelezwa kwa kutumia mfumo tendaji. "Mambo yote yametokea" au "Mungu huyafanya mambo yote yatimie". # kila kitu Kirai cha "kila kitu" kinamaanisha kila kitu kilicho kwenye sheria. "kila kitu kilicho kwenye sheria" au " kila kilichoandikwa kwenye sheria".