# Mnajua hili Yaweza kumaanisha 1) "mnajua hili" kama amri, kuwa makini juu ya lile ninalotaka kuwaandikia au 2) "mnajua hili" kama sentensi kwamba ninataka kuwakumbusha juu ya jambo ambalo mnalijua. # Kila mmoja anapaswa kuwa mwepesi wa kusikia, siyo mwepesi wa kuongea Watu wanapaswa kusikiliza kwa makini na kuzingatia maneno haya " usiwe mwepesi kuongea" haimaanishi uongee taratibu. # si mwepesi wa hasira "usishikwe na hasira mapema" # hasira ya mwanadamu haiwezi kutenda haki ya Mungu Mtu anapokuwa na hasira hawezi kufanya kazi ya Mungu, ambayo ni haki. # wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote Dhambi na ubaya vimezungumzwa hapa kama vitu ambavyo vinapaswa kuwekwa mbali au kutupwa. # wekeni mbali uchafu wa dhambi na ubaya wote Hapa uchafu wa dhambi na ubaya vinamaanisha kitu kimoja. Yakobo ameyatumia kusisitiza ni kwa jinsi gani dhambi ilivyo mbaya. "Acheni kufanya aina zote za dhambi" # uchafu wa dhambi Hapa uchafu inamaanisha dhambi na ubaya. # Kwa unyenyekevu "Bila kujivuna" au "bila kiburi" # lipokeeni neno lililopandwa Neno "kupanda" linamaandishwa kuweka kitu flani ndani ya kitu kingine. Hapa neno la Mungu limetumika kama mmea ambao unapaswa kukua ndani ya waamini. "Utii ujumbe wa Mungu aliousema kwako" # lipokeeni neno lililopandwa "Neno" linamaanisha neno la Mungu linalosimama kama ujumbe wa ukombozi ndani ya Yesu Kristo ambapo Mungu anawaambia waamini. Wakiliamini, Mungu atawaokoa. # kuokoa roho zenu "Awaokoe ninyi toka kwenye hukumu ya Mungu" # roho Hapa neno "roho" inamaanisha mtu.