# Panda katika mlima wa juu, Sayuni, mletaji wa habari njema Mwandishi anazungumzia Sayuni kana kwamba ilikuwa mjumbe anayetmka habari njema kutoka katika kilele cha mlima. # Panda katika mlima wa juu Wajumbe mara kwa mara husimama juu ya nchi iliyoinuka, kama vile milima, ili kwamba watu wengi waweze kusikia kile walichotangaza. # Sayuni Hii ina maana ya watu ambao wanaishi Sayuni. "nyie watu wa Sayuni" # Yerusalemu. Wewe uletaye habari njema Mwandishi anazungumzia Yerusalemu kana kwamba ilikuwa mjumbe ambaye hutangaza habari njema. # na mkono wake wa nguvu hutawala kwa ajili yake Hapa neno "mkono" linawakilisha nguvu ya Mungu. "na anatawala kwa nguvu kubwa" # dhawabu yake ipo pamoja naye ... wale ambao amewaokoa huenda mbele zake Misemo hii miwili ina maana moja. Wale ambao aliwaokoa ni "zawadi" yake. "anawaleta wale aliowaokoa pamoja naye kama zawadi yake"