# Maelezo ya Jumla Hezekia anaendelea maombi yake ya maandishi. # na maisha yangu yarudishwe kwangu Hii inaweza kuelezwa katika hali ya kutenda. "na unipatiea uhai wangu kwangu" # kutoka katika shimo la uharibifu Hezekia hakufa lakini alikuwa karibu ya kufa. Hii ina maana Yahwe kumuokoa katika kufa. Maana kamili ya kauli hii inaweza kuwekwa wazi. "kutoka katika kifo na kwenda katika shimo la uharibifu" au "ili kwamba nisiweze kufa" # kwa kuwa umezitupa dhambi zangu nyuma ya mgongo wako Hezekia anazungumzia Yahwe kusamehe dhambi zake kana kwamba zilikuwa vitu ambavyo Yahwe alitupa nyuma yake na kuvisahau. "kwa maana umesahau dhambi zangu zote na hauvifikirii tena"