# Taarifa ya Jumla: Musa anazungumza wimbo wa shairi kwa watu wa Israeli. # Alimfanya aendeshe katika maeneo ya juu ya nchi Hii ni lahaja. Neno "alimfanya" ina maana ya watu wa Israeli. "Yahwe aliwafanya waendeshe juu sehemu za juu ya nchi" au "Yahwe aliwasaidia kuchukua na kukaa juu ya nchi" # Alimfanya aendeshe ... alimlisha ... alimrutubisha Musa anaendelea kuzungumza na Waisraeli kama "Yakobo" (32:9). Unaweza kutafsiri hiki kana kwamba Musa alikuwa akizungumzia Waisraeli kama watu wengi. "alifanya mababu zetu kuendesha ... aliwalisha .. aliwarutubisha" # alimlisha matunda ya mbugani "alimleta katika nchi ya mazao mengi awezavyo kula" # alimrutubisha kwa asali kutoka kwenye jiwe, na mafuta kutoka kwenye mwamba mgumu sana Nchi ilikuwa na nyuki pori nyingi, ambazo hutoa asali, pamoja na mzinga wa nyuki ndani ya mashimo ya mawe. Kulikuwa na miti mingi ya mizeituni, ambayo hutoa mafuta, na huota juu ya mawe, vilima na milima. # alimrutubisha kwa asali Hii ni kama mama akimpatia mchanga ziwa lake. "alimruhusu kunyonya asali"